Connect with us

Sports

Ligi Kuu Epl;Manchester United Bado mambo Hayajatiki,Everton Wakishinda

Published

on

Kilabu ya Manchester United bado hawajapata ushindi wa Ligi Kuu msimu huu baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Fulham Jumapili, huku kilabu ya Everton ikiongozwa na Jack Grealish ikizindua uwanja wao mpya kwa ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Brighton.

Kikosi cha Ruben Amorim kilikosa nafasi muhimu baada ya Bruno Fernandes kupiga penalti nje kipindi cha kwanza, na United wakatoka na alama moja Craven Cottage.

Goli la kujifunga la Rodrigo Muniz liliwapa United uongozi katika dakika ya 60, lakini Emile Smith Rowe aliingia kama mchezaji wa akiba na kuokoa pointi kwa Fulham akifunga dakika ya 73.

Amorim anajaribu kuinua United baada ya kumaliza msimu uliopita wakiwa nafasi ya 15, lakini safu yake mpya ya ushambuliaji yenye thamani ya £200 milioni (takribani Sh bilioni 35), ikiwajumuisha Matheus Cunha, Bryan Mbeumo na Benjamin Sesko, bado haijazaa matunda.

United walipoteza 1-0 dhidi ya Arsenal kwenye mechi yao ya ufunguzi na sasa watalalamika kupoteza pointi nyingine mbili jijini London.

Fulham, hata hivyo, walihisi wageni walipendelewa na maamuzi mawili tata. Penalti ya United ilitolewa baada ya VAR kuonyesha Calvin Bassey akimvuta Mason Mount, lakini Fernandes alipiga juu ya lango.

Bao lao la kwanza msimu huu lilitokana na kichwa cha Leny Yoro kilichomgonga Muniz na kuingia wavuni, lakini Fulham walikasirishwa VAR kutokuchukua hatua baada ya Bassey kusukumwa.

Smith Rowe alihakikisha Fulham wanapata alama moja baada ya kukamilisha krosi ya Alex Iwobi dakika 17 kabla ya mpira kuisha.


Enzi Mpya ya Everton

Baada ya kuaga kwa hisia uwanja wa Goodison Park, ambao ulikuwa nyumbani kwao tangu mwaka 1892, Everton wanatarajia uwanja wao mpya wenye uwezo wa watazamaji 53,000 kuwarejeshea siku zao za heshima.

Ingawa Everton wameshinda mataji tisa ya ligi kuu — idadi inayopitwa na vilabu vinne pekee — hawajashinda kombe kubwa kwa miaka 30, wakimaliza misimu ya mwisho Goodison wakipambana na kushuka daraja.

“Tunajaribu kusogeza klabu mbele. Hii ni hatua kubwa kwa Everton,” alisema kocha David Moyes.

Grealish, usajili maarufu wa Moyes, alionyesha kipaji kilichomfanya Man City kumlipia Aston Villa £100 milioni mwaka 2021, akipiga pasi za magoli yote mawili.

Iliman Ndiaye, aliyefunga bao la mwisho Goodison mwezi Mei dhidi ya Southampton, aliandika historia nyingine kwa kufunga bao la kwanza kwenye uwanja mpya katika dakika ya 23 baada ya krosi kali ya Grealish.

Brighton walipoteza nafasi nyingi — Kaoru Mitoma akipiga mwamba, Jan Paul van Hecke kugonga nguzo na Danny Welbeck akikosa bao wazi.

James Garner aliongeza la pili mapema kipindi cha pili kwa shuti kali baada ya pasi ya Grealish.

Brighton walipata nafasi ya kufufua matumaini kwa penalti, lakini Jordan Pickford aliokoa mkwaju dhaifu wa Welbeck, na kukamilisha siku ya kumbukumbu kwa Everton.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending