Connect with us

Sports

Ligi Kuu Uingereza EPL Kufungua Milango Yake Hii Leo

Published

on

Huku Ligi Kuu Uingereza ikifungua Milango rasmi hii leo usiku kilabu ya Arsenal watakabiliwa na mtihani wa mapema wa kuonyesha uwezo wao wa kupigania taji dhidi ya Manchester United iliyofanyiwa maboresho siku ya jumapili jioni, huku mabingwa watetezi Liverpool ikizindua uhasama wa  msimu mpya wa Ligi Kuu ya Uingereza nyumbani dhidi ya Bournemouth saa nne usiku.

Newcastle wanatarajiwa kumkosa mshambuliaji wao nyota Alexander Isak, ambaye anataka kuondoka, katika safari ngumu ya ugenini dhidi ya Aston Villa.

Kama Kipenga Cha Coco FM hebu tuangalie kwa undani jinsi timu zimejipanga kuelekea msimu mpya;

Sajili wapya Benjamin Sseko na Victor Gyokeres;Ni washambulizi wawili ambao wengi watakua wanamulika kwa macho ya ndaani kuona jinsi wataongoza safu zao tofauti za mashambulizi,Wawili hao wanatarajiwa kuanza katika timu zao ugani Old Trafford Jumapili hii.

Kilabu ya Arsenal walimumezea mate mshambulizi Sseko akiwa na RB Leipzig kwa zaidi ya mwaka mmoja kabila badaye kumsajili mshambulizi Victor Gyokeres kwa pauni milioni 64.9 kutoka Sporting Lisbon nyota ambaye pia alikua chaguo la kocha Ruben Amorim wa United kwani waliwahi kufanya kazi pamoja.

Vijana wa Mikel Arteta wakiwa wamemaliza misimu mitatu mfululizo bila kushinda taji la EPL wakisaka mfungaji wa kuwasaidia kufunga zaidi.Na mtu wa kuwapa matumaini hayo ni Gyokeres ambaye katika miaka 2 Sporting alifanikiwa kufunga magoli 97 katika mechi 102.

United msimu jana walikua timu mbovu wakimaliza nafasi ya 15 ligi ya Uingereza kwa mara ya kwanza chini ya Amorim ila sasa wamefanya mabadiliko ikiwemo kusajili nyota Matheus Cunha na Bryan Mbeumo wote ambao walingaa msimu jana na Wolves na Brenford Mtawalia.

Ligi hiyo inpoanzaa leo macho ni kwa Liverpool ambayo licha ya kuwa mabingwa na kuondokewa na badhi ya nyota ikiwemo Alexander Trent Arnold,Luis Diaz na Darwin Nunez wameimarisha kikosi chao kupitia kiungo Florian Wirtz kwa pauni milioni 116,beki Jeremie Frimpong na mshambulizi Hugo Ekitite wakivunja rekodi ya matumizi hadi pauni milioni 260 kwa msimu mmoja.

Wakati vilabu vikuu sita na za jadi  Ligi Kuu ya Uingereza—Liverpool, Manchester City, Manchester United, Arsenal, Chelsea na Tottenham—zinavyoendelea kutumia nguvu zao za kifedha kwenye soko la usajili, Aston Villa na Newcastle zimejikuta zikisukumwa pembeni.

Kwa kuwa na vizuizi vya kanuni za uendelevu wa kifedha, usajili mkubwa pekee wa Villa umekuwa ni mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Evann Guessand, aliyejiunga kutoka Nice.

Kocha wa Newcastle, Eddie Howe, amekuwa akipokea maswali ya mara kwa mara kuhusu hali ya Alexander Isak, ambaye alisusia maandalizi ya msimu mpya akilazimisha uhamisho anaoutamani kwenda Liverpool.

Juhudi za The Magpies kumpata mbadala wa mshambuliaji huyo wa Kiswidi zimegonga mwamba mara kwa mara, huku wachezaji kama Sesko, Mbuemo, Hugo Ekitike, Liam Delap na Joao Pedro wakiamua kujiunga na timu nyingine.

Hata hivyo, katika misimu ya hivi karibuni, Villa na Newcastle wamekuwa wakifanya vizuri zaidi kuliko baadhi ya klabu sita kubwa na msimu huu pia wamelenga kufuzu tena kwa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Ijumaa;

Liverpool v Bournemouth 22:00pm

Jumamosi;

Aston Villa v Newcastle (5:30pm), Brighton v Fulham, Sunderland v West Ham, Tottenham v Burnley, Wolves v Man City (7:30pm)

Jumapili;

Chelsea v Crystal Palace, Nottingham Forest v Brentford (4:00pm), Man Utd v Arsenal (6:30pm)

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending