Connect with us

Sports

Lionel Messi Astaafu Licha ya kufunga mabao mawili akiiongoza Argentina, huku Uruguay, Colombia na Paraguay wakifuzu Kombe la Dunia 2026

Published

on

Mshambulizi Lionel Messi alifunga mara mbili kwa Argentina katika mazingira ya kihisia jijini Buenos Aires siku ya Alhamisi, huku Uruguay, Colombia na Paraguay wakijiunga na mabingwa watetezi kwenye Kombe la Dunia mwakani ambapo pia alitangaza kustaafu kuchezea taifa hilo.

Katika mechi yake ya mwisho ya kufuzu akiwa nyumbani kwa taifa lake, na Argentina tayari wakiwa wamepata nafasi yao Amerika Kaskazini, Messi alifunga dakika ya 39 na 80 na kuipa timu yake ushindi wa 3-0 dhidi ya Venezuela.

Messi, mshindi wa Ballon d’Or mara nane, aling’aa mbele ya mashabiki 80,000 waliokuwa wamefurika kwenye uwanja wa Mas Monumental, akionyesha bado ana ubora wa juu. Nyota huyo wa Argentina atatimiza miaka 39 wakati wa Kombe la Dunia lijalo, lakini licha ya umri wake mkubwa, anaonekana kuwa bado atakuwa na nafasi muhimu katika kutetea taji la Lionel Scaloni. Scaloni amethibitisha kwamba nahodha wake atapumzishwa kwa mechi isiyo na maana wiki ijayo dhidi ya Ecuador.

“Ametoa juhudi kubwa mno na anastahili kupumzika na pia kuwa na familia yake,” alisema kocha.
“Alimaliza akiwa amechoka sana kimwili. Alipaswa kutoka, lakini hakutaka kwa sababu ya hali ya kihisia ya mechi.”

Messi aliingia uwanjani akiwa na watoto wake watatu kabla ya kuanza mchezo, huku pia baba yake Jorge akihudhuria tukio hilo.

Uruguay walifuzu kwa michuano ya Marekani, Kanada na Mexico baada ya kuifunga Peru 3-0 nyumbani, huku Colombia wakiifunga Bolivia kwa matokeo sawa.

Paraguay pia walipata nafasi ya kushiriki fainali za 2026 baada ya kutoka sare ya 0-0 nyumbani dhidi ya Ecuador ambao tayari walikuwa wamefuzu.

Brazil, ambao walikuwa tayari wamefuzu, waliibamiza Chile 3-0 kwenye Maracana, huku wachezaji wa Ligi Kuu ya England Estevao, Lucas Paqueta na Bruno Guimaraes wakifunga mabao.
Hilo lilikuwa bao la kwanza kwa Estevao, winga wa Chelsea mwenye umri wa miaka 18, akiwa na timu ya taifa.

  • Bielsa afanikisha tena

Mbele ya mashabiki 60,000 kwenye Estadio Centenario mjini Montevideo, Rodrigo Aguirre aliwaweka Uruguay wa Marcelo Bielsa kifua mbele dakika ya 14.
Mshambuliaji huyo wa Club America aliruka juu na kupiga kichwa cha nguvu kilichoenda moja kwa moja kona ya juu, akimwacha kipa wa Peru Pedro Gallese hana la kufanya.

Wauruguay, mabingwa wa Kombe la Dunia 1930 na 1950, walihitaji pointi moja pekee kufuzu na kumpeleka kocha wao mkongwe Marcelo Bielsa kwenye fainali nyingine.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 70 sasa ameifikisha timu yake ya tatu kufuzu Kombe la Dunia.

Kuteuliwa kwa Bielsa kama kocha wa Uruguay mwaka 2023 kulipokelewa kwa shauku na furaha kubwa, lakini kampeni yao ya kufuzu isiyovutia ilipunguza matarajio hayo.

Hata hivyo, kufuzu kwao kulitarajiwa kutokana na mfumo mpya unaoruhusu timu sita kati ya 10 za CONMEBOL kufuzu moja kwa moja kwa 2026, huku timu nyingine moja ikielekea mchujo wa mabara.

Kwa sasa Venezuela wako nafasi ya saba wakiwa na mechi moja zaidi ya kufuzu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending