Connect with us

Sports

Mabingwa wa Kenya akina Dada Police Bullets watinga Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa wa Afrika Kanda ya CECAFA.

Published

on

Magoli mawili kutoka kwa Emily Moranga na Mganda Zaina Namileme yaipa Kenya Police Bullets ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya miamba wa Eritrea, DenDen FC, na kutinga nusu fainali za kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Afrika Kanda ya CECAFA.

Mechi hiyo iliyochezwa katika Uwanja wa Nyayo Jumatano alasiri ilishuhudia mabingwa wa Kenya wakichukua ushindi wao wa pili mfululizo katika hatua ya kufuzu, baada ya kuanza kampeni kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Kampala Queens ya Uganda Alhamisi iliyopita.

Ushindi huo sasa unaweka timu hiyo ya maafisa wa polisi kileleni mwa Kundi A wakiwa na alama 6, tatu mbele ya Kampala Queens huku DenDen wakiwa hawajapata ushindi wowote katika mechi za makundi. Kipigo hicho pia kiliwaondoa mabingwa hao wa Eritrea kwenye mashindano, baada ya kubamizwa 7-0 na Kampala Queens katika mechi yao ya ufunguzi.

Police walitarajiwa kushinda kwa mabao mengi zaidi lakini Elizabeth Ochaka alipiga shuti lililogonga mwamba dakika ya 36.

Nafasi nyingine ya moja kwa moja ilijitokeza dakika ya 50 kipindi cha pili baada ya mchezaji wa akiba Vidah Okeyo kupiga shuti la mbali lililoondolewa vyema na kipa Sofanit Gebresilasie.

DenDen walionekana kucheza mchezo wa kujilinda katika kipindi cha kwanza, lakini nafasi yao ya kufunga ilijitokeza dakika ya 62 baada ya mshambuliaji Rahwa Hans kupiga shuti lililoelekezwa langoni, lakini kipa wa Police, Annedy Kundu, alipangua kwa ustadi.

Kocha Odemba alifanya mabadiliko kadhaa kwa kuwaleta Sharon Vidah, Purity Anyetu, Rebecah Odato na Lucy Jirah, waliowachukua nafasi Margaret Kunihira, Zainab Namileme, Lourna Nyabuto na Leah Cherotich.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending