Connect with us

Sports

Makala ya mbio za magari WRC kufikia Tamati Jumapili Hii

Published

on

Maelfu ya mashabiki kutoka afrika mashariki na kati wamiminika mjini Naivasha kaunti ya Nakuru kwa mbio za magari ya WRC Makala ya mwaka 2025.

Kwa mujibu wa waandalizi Zaidi ya mashabiki 30,000 wametua jijini humo kutoka mataifa ya Uganda,Tanzania na Rwanda kwa mbio hizo ambazo zilianza rasmi siku ya alhamisi jijini Nairobi.

Eflyn Evans dereva kutoka taifa la Wales ndio anaongeza akitumia gari aina ya Toyota Gazoo muda sekunde 46.1 baada ya raundi ya pili akifuatwa na bingwa mara mbili Kalle Rovanpera raia wa uhispania akitumia Toyota pia watatu ni Ottok Tanak raia wa Estonia ambaye anatumia gari aina ya Hyundai Shell Mobis.

Dereva anayeongoza mpaka sasa dereva Eflyn Evans na msaidizi wake Scott Martin alikua na haya yakusema baada ya kuchukua uongozi wa mapmea.

“Plan yetu ilifanya kazi vizuri,tunafuraha kuchukua uongozi wa mapema ila bado kazi ipo kwani mizungumzo ni minane,tutaona itakavyokua mpaka siku ya mwisho.”

Kwa upande wake dereva nambari mbili na bingwa mtetezi Kalle Rovanpera na msaidizi wake Jonne Halttunen alisema haya baada ya kushindwa;

“Leo haikua siku nzuri kwetu tulitumia muda mwingi asubuhi ila bado safari ya sisi kurejea kileleni.”

Naye dereva namba tatu Ott Tanak aliyasema haya;

“Hauwezi ukapanga kusema kweli ukiwa hapa kenya vitu vingi vinafanyika,Ni lazima tuketi chini tufahamu tatizo ambalo linatukumba na gari letu.”

Raundi ya tatu na nne yanaishwa maeneo ya Elmentaita huku jumapili mbio hizo zikiisha Hells Gate 1 na Hells GATE 2.

Kilele cha mbio hizo ni siku ya jumapili ambapo rais William Samoei Ruto anatarajiwa kufunga mbio hizo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending