Sports
Makala ya mbio za magari WRC kufikia Tamati Jumapili Hii
Maelfu ya mashabiki kutoka afrika mashariki na kati wamiminika mjini Naivasha kaunti ya Nakuru kwa mbio za magari ya WRC Makala ya mwaka 2025.
Kwa mujibu wa waandalizi Zaidi ya mashabiki 30,000 wametua jijini humo kutoka mataifa ya Uganda,Tanzania na Rwanda kwa mbio hizo ambazo zilianza rasmi siku ya alhamisi jijini Nairobi.
Eflyn Evans dereva kutoka taifa la Wales ndio anaongeza akitumia gari aina ya Toyota Gazoo muda sekunde 46.1 baada ya raundi ya pili akifuatwa na bingwa mara mbili Kalle Rovanpera raia wa uhispania akitumia Toyota pia watatu ni Ottok Tanak raia wa Estonia ambaye anatumia gari aina ya Hyundai Shell Mobis.
Dereva anayeongoza mpaka sasa dereva Eflyn Evans na msaidizi wake Scott Martin alikua na haya yakusema baada ya kuchukua uongozi wa mapmea.
“Plan yetu ilifanya kazi vizuri,tunafuraha kuchukua uongozi wa mapema ila bado kazi ipo kwani mizungumzo ni minane,tutaona itakavyokua mpaka siku ya mwisho.”
Kwa upande wake dereva nambari mbili na bingwa mtetezi Kalle Rovanpera na msaidizi wake Jonne Halttunen alisema haya baada ya kushindwa;
“Leo haikua siku nzuri kwetu tulitumia muda mwingi asubuhi ila bado safari ya sisi kurejea kileleni.”
Naye dereva namba tatu Ott Tanak aliyasema haya;
“Hauwezi ukapanga kusema kweli ukiwa hapa kenya vitu vingi vinafanyika,Ni lazima tuketi chini tufahamu tatizo ambalo linatukumba na gari letu.”
Raundi ya tatu na nne yanaishwa maeneo ya Elmentaita huku jumapili mbio hizo zikiisha Hells Gate 1 na Hells GATE 2.
Kilele cha mbio hizo ni siku ya jumapili ambapo rais William Samoei Ruto anatarajiwa kufunga mbio hizo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

