Connect with us

Sports

Martinelli Aokoa Arsenal Kwa Bao la Dakika Za Jioooni Dhidi ya Man City

Published

on

Goli la kusawazisha la Gabriel Martinelli dakika ya 93 liliokoa matumaini ya Arsenal ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuepuka kichapo dhidi ya Manchester City, huku Aston Villa ikiendelea bila ushindi baada ya sare tasa ya 1-1 dhidi ya Sunderland waliokuwa na wachezaji 10.

The Gunners walikuwa wanakaribia kupoteza mara ya pili katika mechi tano za Ligi Kuu baada ya Erling Haaland kuwafungia City bao la mapema kupitia shambulizi la kushtukiza.

Martinelli alitokea benchi na kufunga kwa mara ya pili ndani ya wiki moja kuokoa sare ya 1-1, lakini timu zote mbili zikapoteza nafasi ya kusogea karibu na vinara Liverpool.

“Nimevunjika moyo sana kwa kutoshinda,” alisema kocha wa Arsenal, Mikel Arteta. “Nafikiri tulicheza vizuri zaidi kuliko mwaka jana tulipowafunga (5-1).”

Arsenal walikuwa hawajaruhusu bao lolote la wazi katika mechi zao tano za mwanzo za Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa msimu huu, lakini walipenya dakika ya tisa kupitia mfungaji bora zaidi duniani kwa sasa.

Haaland alianza shambulizi ndani kabisa ya nusu yao kwa kumpasia Tijjani Reijnders kisha akakimbia kwa kasi kupokea pasi ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi kabla ya kumtuliza kipa David Raya kwa ustadi.

Mnorwe huyo tayari ana mabao 13 kwa klabu na taifa ndani ya mechi nane pekee msimu huu.

Upande wa pili, City wameanza kufaidika mara moja na usajili wa kipa mrefu wa Kiitaliano, Gianluigi Donnarumma.

Shuti kali la Noni Madueke lililolenga lango liliokolewa kwa ustadi na Donnarumma katika jaribio bora zaidi la Arsenal kipindi cha kwanza.

Arteta aliwaingiza wachezaji wabunifu Bukayo Saka na Eberechi Eze mwanzoni mwa kipindi cha pili.

Eze alimjaribu tena Donnarumma, lakini Gunners walihangaika kuivunja ngome ya ulinzi ya City, huku Guardiola hata akimtoa Haaland na Phil Foden kipindi cha pili ili kuimarisha safu ya ulinzi.

Hata hivyo, dau hilo halikufanikiwa baada ya Martinelli kuparamia mpira wa juu kutoka kwa Eze na kumpiga Donnarumma kwa mkwaju wa kuvutia uliopinda juu yake.

“Sio kwamba tunataka kuwa hivi, lakini wakati mpinzani ni bora zaidi, tunalazimika kujilinda kwa kina na kushambulia kwa kushtukiza,” alisema Guardiola.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending