Sports
Mashemeji Derby: Gor kumenyana na Afc Raila Odinga Stadium
Mashemeji Derby
Kilabu ya Gor Mahia kuzindua uhasama na watani wao wa tangu jadi kilabu ya Afc Leopards katika debi la 97 leo uwanjani Raila Odinga Stadium mjini Homabay.
Mtanange huo ni kufa kupona kwa Kogalo ambao wana shinikizo za kupata alama zote tatu ili kuweka hai matumaini ya kutetea ubingwa wa ligi kuu Fkf Premier Ligi msimu huu.
Kwa Mujibu wa kocha mshikilizi wa Sirkali Zedekiah Zico Otieno mechi ya debi haina mwenyewe ila watacheza kwa ubora zaidi kupata ushindi.
“Kila mtu anajua debi huwa ngumu na haina mwenyewe,tunaenda kucheza kwa mfumo wa kushinda mechi hii na kupata alama tatu muhimu kwani ndio lengo letu kuu,Hata hivyo ni lazima mashabiki wawe tayari kwa matokeo yoyote kwani katika soka kuna kushinda,sare na kupoteza”.
Gor Mahia wanashikilia nafasi ya tatu kwenye jedwali la ligi kuu na alama 54 kutokana na mechi 31 huku Ingwe ikiwa ya sita na alama 46.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

