Connect with us

Sports

Mashindano ya CHAN 2024 Yaingia Hatua Robo Fainali

Published

on

Mashindano ya TotalEnergies African Nations Championship (CHAN) 2024 yameingia hatua ya robo fainali baada ya mechi za mwisho za makundi kukamilika hapo jana kwa msisimko mkubwa.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya CAF, mashindano makubwa yameandaliwa kwa pamoja na mataifa matatu β€” Kenya, Tanzania na Uganda β€” na yote yamefuzu robo fainali, jambo linaloendeleza hamasa kubwa ya mashindano haya barani.

Ufanisi wa wenyeji umeongeza uzito zaidi kwa kaulimbiu ya mashindano haya, β€œPamoja,” huku Afrika Mashariki ikijiandaa kushuhudia raundi nyingine ya viwanja vilivyojaa na mashabiki wenye shauku.

Kenya Yaongoza Kundi A Katika Debut;

Harambee Stars ya Kenya imekuwa moja ya simulizi kuu za mashindano, ikibatilisha matarajio kwa kufuzu robo fainali kwa mara ya kwanza katika historia yake ya CHAN na kuibuka kinara wa Kundi A.

Bao la dakika za mwisho la Ryan Ogam dhidi ya Zambia liliihakikishia Kenya ushindi wa 1-0 na kukamilisha alama 10 kileleni. Kikosi cha Benni McCarthy kimeruhusu bao moja pekee katika mechi nne, kikiashiria uimara wake wa kiulinzi.

Kenya sasa itasalia Nairobi kucheza dhidi ya Madagascar Ijumaa katika Uwanja wa Moi Kasarani. Kwa msaada wa mashabiki wa nyumbani na hali nzuri ya matokeo, Harambee Stars wamebadilika haraka kutoka wanyonge hadi kuwa tishio.

Tanzania Yatinga Robo Fainali Kwa Nguvu

Taifa Stars ya Tanzania pia iliibuka vinara wa Kundi B kwa alama 10, ikipata ushindi mara tatu na sare moja. Kikosi hiki kiliwasisimua mashabiki kwa mashambulizi makali na uthabiti, huku kiporo pekee kikiwa sare dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Tanzania sasa itakutana na Morocco Ijumaa jioni jijini Dar es Salaam. Atlas Lions, mabingwa mara mbili wa CHAN, waliibuka wa pili katika Kundi A nyuma ya Kenya.

Uganda Yavunja Nuksi ya kuondolewa mapema;

Baada ya kushindwa kufuzu hatua ya mtoano mara sita mfululizo, Uganda hatimaye imepiga hatua hadi robo fainali. Sare ya mabao 3-3 dhidi ya Afrika Kusini jijini Kampala iliwatosha Cranes kuibuka vinara wa Kundi C kwa pointi saba. Penalti ya dakika za majeruhi ya Rogers Torach ilisababisha shangwe kubwa katika Uwanja wa Taifa wa Mandela.

Uganda sasa itakutana na Senegal Jumamosi usiku, mechi inayotarajiwa kuvutia umati mkubwa zaidi katika historia ya mashindano haya.

Kundi D Laamuliwa Zanzibar

Huko Zanzibar, Sudan na Senegal zilitoka sare tasa ya 0-0 na zote zikafuzu kutoka Kundi D. Sudan, ambayo haijapoteza chini ya kocha Kwesi Appiah, iliibuka kinara kwa tofauti ya mabao, huku mabingwa watetezi Senegal wakimaliza wa pili.

Sudan itasalia Zanzibar kuvaana na Algeria Jumamosi mchana, huku Senegal wakielekea Kampala kwa mtanange wao wa robo fainali dhidi ya Uganda.


Mechi za Robo Fainali

Ijumaa, 22 Agosti 2025

  • Kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ vs Madagascar πŸ‡²πŸ‡¬ – Saa 11:00 jioni, Uwanja wa Moi Kasarani, Nairobi

  • Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ vs Morocco πŸ‡²πŸ‡¦ – Saa 2:00 usiku, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam

Jumamosi, 23 Agosti 2025

  • Sudan πŸ‡ΈπŸ‡© vs Algeria πŸ‡©πŸ‡Ώ – Saa 11:00 jioni, Uwanja wa Amaan, Zanzibar

  • Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬ vs Senegal πŸ‡ΈπŸ‡³ – Saa 2:00 usiku, Uwanja wa Taifa wa Mandela, Kampala

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development FundΒ (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali MstaafuΒ Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending