Sports
Mashindano ya CHAN 2024 Yaingia Hatua Robo Fainali
Mashindano ya TotalEnergies African Nations Championship (CHAN) 2024 yameingia hatua ya robo fainali baada ya mechi za mwisho za makundi kukamilika hapo jana kwa msisimko mkubwa.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya CAF, mashindano makubwa yameandaliwa kwa pamoja na mataifa matatu β Kenya, Tanzania na Uganda β na yote yamefuzu robo fainali, jambo linaloendeleza hamasa kubwa ya mashindano haya barani.
Ufanisi wa wenyeji umeongeza uzito zaidi kwa kaulimbiu ya mashindano haya, βPamoja,β huku Afrika Mashariki ikijiandaa kushuhudia raundi nyingine ya viwanja vilivyojaa na mashabiki wenye shauku.
Kenya Yaongoza Kundi A Katika Debut;
Harambee Stars ya Kenya imekuwa moja ya simulizi kuu za mashindano, ikibatilisha matarajio kwa kufuzu robo fainali kwa mara ya kwanza katika historia yake ya CHAN na kuibuka kinara wa Kundi A.
Bao la dakika za mwisho la Ryan Ogam dhidi ya Zambia liliihakikishia Kenya ushindi wa 1-0 na kukamilisha alama 10 kileleni. Kikosi cha Benni McCarthy kimeruhusu bao moja pekee katika mechi nne, kikiashiria uimara wake wa kiulinzi.
Kenya sasa itasalia Nairobi kucheza dhidi ya Madagascar Ijumaa katika Uwanja wa Moi Kasarani. Kwa msaada wa mashabiki wa nyumbani na hali nzuri ya matokeo, Harambee Stars wamebadilika haraka kutoka wanyonge hadi kuwa tishio.
Tanzania Yatinga Robo Fainali Kwa Nguvu
Taifa Stars ya Tanzania pia iliibuka vinara wa Kundi B kwa alama 10, ikipata ushindi mara tatu na sare moja. Kikosi hiki kiliwasisimua mashabiki kwa mashambulizi makali na uthabiti, huku kiporo pekee kikiwa sare dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Tanzania sasa itakutana na Morocco Ijumaa jioni jijini Dar es Salaam. Atlas Lions, mabingwa mara mbili wa CHAN, waliibuka wa pili katika Kundi A nyuma ya Kenya.
Uganda Yavunja Nuksi ya kuondolewa mapema;
Baada ya kushindwa kufuzu hatua ya mtoano mara sita mfululizo, Uganda hatimaye imepiga hatua hadi robo fainali. Sare ya mabao 3-3 dhidi ya Afrika Kusini jijini Kampala iliwatosha Cranes kuibuka vinara wa Kundi C kwa pointi saba. Penalti ya dakika za majeruhi ya Rogers Torach ilisababisha shangwe kubwa katika Uwanja wa Taifa wa Mandela.
Uganda sasa itakutana na Senegal Jumamosi usiku, mechi inayotarajiwa kuvutia umati mkubwa zaidi katika historia ya mashindano haya.
Kundi D Laamuliwa Zanzibar
Huko Zanzibar, Sudan na Senegal zilitoka sare tasa ya 0-0 na zote zikafuzu kutoka Kundi D. Sudan, ambayo haijapoteza chini ya kocha Kwesi Appiah, iliibuka kinara kwa tofauti ya mabao, huku mabingwa watetezi Senegal wakimaliza wa pili.
Sudan itasalia Zanzibar kuvaana na Algeria Jumamosi mchana, huku Senegal wakielekea Kampala kwa mtanange wao wa robo fainali dhidi ya Uganda.
Mechi za Robo Fainali
Ijumaa, 22 Agosti 2025
-
Kenya π°πͺ vs Madagascar π²π¬ β Saa 11:00 jioni, Uwanja wa Moi Kasarani, Nairobi
-
Tanzania πΉπΏ vs Morocco π²π¦ β Saa 2:00 usiku, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam
Jumamosi, 23 Agosti 2025
-
Sudan πΈπ© vs Algeria π©πΏ β Saa 11:00 jioni, Uwanja wa Amaan, Zanzibar
-
Uganda πΊπ¬ vs Senegal πΈπ³ β Saa 2:00 usiku, Uwanja wa Taifa wa Mandela, Kampala
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development FundΒ (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali MstaafuΒ Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

