Connect with us

Sports

Mashindano ya kandanda ya Kombe la Dola yamezinduliwa rasmi hii leo katika kaunti ya Mombasa.

Published

on

Mashindano ya kandanda ya kombe la Dola yamezinduliwa rasmi hii leo mjini Mombasa.

Mashindano hayo ambayo yanajumuisha timu ishirini kutoka kaunti za Mombasa, Kwale na Kilifi, yanatarajiwa kufanyika kwa kipindi cha mwezi mmoja katika uwanja wa Mombasa Sports Club.

Akizungumza na wanahabari, Afisa wa Mawasiliano wa Kampuni ya Dola, Hassan Ibrahim, amesema mashindano haya yamelenga kuwapa vijana fursa ya kuonyesha vipaji vyao, pamoja na kuwaweka katika nafasi nzuri ya kujikuza kisoka.

Aidha amebainisha kuwa mshindi wa mashindano haya atajinyakulia kitita cha shilingi nusu milioni, huku timu zitakazomaliza katika nafasi ya pili hadi ya nne zikijishindia zawadi ya kati ya shilingi laki mbili na nusu hadi elfu hamsini.

Aidha, wachezaji binafsi watakaoonyesha kiwango cha juu cha mchezo watatunukiwa shilingi elfu ishirini kila mmoja.

“Leo tunaanza ukurasa mpya wa makala ya mwaka huu kombe la SISINIDOLA Kaunti za Mombasa,kwale na Kilifi,Mshindi atapokea nusu milioni naye wa pili mpaka nafasi ya nne watanufaika na pesa hadi laki mbili wa nafasi ya nne kando na wachezaji kutuzwa.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka FKF Kaunti ya Mombasa, Allamin Abdallah, amewataka vijana wanaoshiriki kutumia nafasi hiyo kama jukwaa la kujitangaza na kujiendeleza kisoka.

“mashindano haya ni fursa kwa vijana kuonyesha uwezo walio nao kwani ukanda wa pwani inajulikana kwa mapenzi ya dhati kwa soka .”

Nao Kocha Rajab Babuu, ambaye ni msimamizi wa Mombasa Sports Club, amemtaka mfadhili wa mashindano hayo kuhakikisha kuwa wanawafuata kwa karibu wachezaji watakaoibuka na vipaji, ili kuwapa mwongozo na kuwaendeleza katika taaluma yao ya kandanda.

“Haya mashindani ni jambo zuri kwa vijana wetu na naomba mfadhili wetu wafuatilie vijana ili vipaji vyao pamoja na values ziwe katika hali shwari.”

Meshi hizo zimeongoa nanga rasmi uwanjani Mombasa Sports Club hii leo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending