Sports
Mashindano Ya Shule Ya Upili Yaanza Kwa Kishindo Pwani
Mabingwa watetezi wa soka kwa shule za upili eneo la Likoni Moi Forces Academy walianza vyema kampeni ya kutetea taji lao kwa kupata ushindi katika mechi zao zote za makundi.
Katika mechi ya kwanza waliitandika shule ya upili ya Likoni Boyz 2-0 kisha wakawageukia Timbwani na kuwatandika 4-0.
Katika mechi zingine kwenye kundi A, shule ya upili ya Mrima iliitandika Likoni Boys goli 1-0 huku Shikaadabu ikiigaragaza Tibwani magoli 2-0 na kwenye mechi ya pili Mrima ikapigwa magoli 3-1 na Shikaadabu.
Katika kundi B, shule ya upili ya Puma iliilambisha Mwahima magoli 2-1, huku Ushindi ikiilaza Al-Miraj magoli 3-0,nayo Bububu ikipata magoli 2-0 dhidi ya Al- Miraj na katika mechi ya pili Puma ikitoka sare ya 0-0 dhidi ya Ushindi nayo Bubububu ikicharazwa magoli 2-0 na Mwahima.
Katika upande wa akina dada, Kundi A, shule ya upili ya MFGA ilianza vyema kwa kujinyakulia magoli 7-0 dhidi ya Puma, kisha katika mechi ya pili ikaicharazwa na Mishi Mboko magoli 4-0, kisha Mishi Mboko ikailaza Shikaadabu magoli 3-0 na katika mechi ya pili Shikaadabu ikatoka 2-1 dhidi ya Puma.
Katika kundi B, Timwani ilitoka 1-0 dhidi ya Mtongwe Girls, na mechi ya pili Timbwani ikacharazwa 2-0 na Mwahima, nayo Ushindi ikatoka sare ya goli 1-1 na Mwahima, na kisha Mtongwe ikasawazisha mchezo kwa sare ya 0-0 dhihi ya Ushindi.
Kwenye matokeo ya malindi sub county
Barani sec 3-0 Lango BAYA
Canon 0-1 Ganda sec
Barani 1-0 Ganda
Langobaya 2-2 Canon
Malindi 2-0 Bishop Kalu
Gede sec 0-4 Malindi High
Gede 2-0 Bishop Kalu
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

