Connect with us

Sports

Mashindano Ya Shule Ya Upili Yaanza Kwa Kishindo Pwani

Published

on

Mabingwa watetezi wa soka kwa shule za upili eneo la Likoni Moi Forces Academy walianza vyema kampeni ya kutetea taji lao kwa kupata ushindi katika mechi zao zote za makundi.

Katika mechi ya kwanza waliitandika shule ya upili ya Likoni Boyz 2-0 kisha wakawageukia Timbwani na kuwatandika 4-0.

Katika mechi zingine kwenye kundi A, shule ya upili ya Mrima iliitandika Likoni Boys goli 1-0 huku Shikaadabu ikiigaragaza Tibwani magoli 2-0 na kwenye mechi ya pili Mrima ikapigwa magoli 3-1 na Shikaadabu.

Katika kundi B, shule ya upili ya Puma iliilambisha Mwahima magoli 2-1, huku Ushindi ikiilaza Al-Miraj magoli 3-0,nayo Bububu ikipata magoli 2-0 dhidi ya Al- Miraj na katika mechi ya pili Puma ikitoka sare ya 0-0 dhidi ya Ushindi nayo Bubububu ikicharazwa magoli 2-0 na Mwahima.

Katika upande wa akina dada, Kundi A, shule ya upili ya MFGA ilianza vyema kwa kujinyakulia magoli 7-0 dhidi ya Puma, kisha katika mechi ya pili ikaicharazwa na Mishi Mboko magoli 4-0, kisha Mishi Mboko ikailaza Shikaadabu magoli 3-0 na katika mechi ya pili Shikaadabu ikatoka 2-1 dhidi ya Puma.

Katika kundi B, Timwani ilitoka 1-0 dhidi ya Mtongwe Girls, na mechi ya pili Timbwani ikacharazwa 2-0 na Mwahima, nayo Ushindi ikatoka sare ya goli 1-1 na Mwahima, na kisha Mtongwe ikasawazisha mchezo kwa sare ya 0-0 dhihi ya Ushindi.

Kwenye  matokeo ya malindi sub county

Barani sec 3-0 Lango BAYA

Canon 0-1 Ganda sec

Barani 1-0 Ganda

Langobaya 2-2 Canon

Malindi 2-0 Bishop Kalu

Gede sec 0-4 Malindi High

Gede 2-0 Bishop Kalu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending