Connect with us

Sports

Michezo ya Walemavu wa Usikivu 2025: Majaribio ya Kitaifa ya Mpira wa Kikapu Yaangazia Vipaji Vipya Kenya

Published

on

Mbio za kutafuta wawakilishi wa Kenya katika Michezo ya Walemavu wa Usikivu (Deaflympics) 2025 jijini Tokyo, Japani kuanzia Novemba 15 hadi 26, zilianza hapo jana kwa majaribio ya kitaifa ya mpira wa kikapu yaliyowaleta pamoja wachezaji kutoka kaunti saba katika Uwanja wa USIU.

Majaribio hayo ya siku mbili yanalenga kuchagua wachezaji 20 ambao wataingia kambini kabla ya kupunguzwa hadi kikosi cha mwisho cha wachezaji 12.

Kaunti zinazoshiriki ni pamoja na Nairobi, Mombasa, Kwale, Nakuru, Kericho, Kisumu na Nyeri. Tukio hili tayari limevutia vipaji vya hali ya juu, huku wachezaji chipukizi kuanzia umri wa miaka 17 wakijitosa uwanjani wakitaka kupata nafasi ya kuingia timu ya taifa.

Kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Kenya, Mary Chepkoi, alielezea furaha yake kutokana na kiwango cha ushindani na ujio wa vipaji vipya.

“Nina furaha kuwa majaribio haya yameleta sura mpya. Mustakabali ni mzuri kwa timu itakayochaguliwa,” alisema, akisisitiza umuhimu wa kujenga wingi wa wachezaji na mwendelezo wa kizazi kipya.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu kwa Viziwi Kenya, Gilbert Ogolla, alikiri changamoto za kuendesha majaribio bila wafadhili wa nje, wakitegemea zaidi michango ya wanachama.

“Haijakuwa rahisi, lakini tumeweza kwa kugawanya majukumu ndani ya shirikisho. Tunatumai kwamba timu itakapoingia kambini, tutapata msaada zaidi kutoka kwa serikali na wadau wengine,” alisema Ogolla.

Miongoni mwa wanaowania nafasi ya kwenda Tokyo ni Mercy Mideva, kiongozi wa timu kutoka Kajiado ambaye aliwakilisha Kenya kwenye Michezo ya Walemavu wa Usikivu Brazil 2023.

“Lengo langu ni kufanya kazi kwa bidii na kuingia katika timu ya mwisho. Tutatumia uzoefu wa Michezo ya Olimpiki 2022 ili kusukuma matokeo bora zaidi Tokyo,” alisisitiza.

Kenya inaingia katika Michezo ya Walemavu wa Usikivu 2025 ikiwa na matumaini mapya, baada ya Kamati ya Kimataifa ya Michezo kwa Walemavu wa Usikivu (ICSD) kuondoa adhabu yake mapema mwaka huu.

Marufuku hiyo ilikuwa imewekwa baada ya nchi kushindwa kutuma timu kwenye Mashindano ya Dunia ya Mpira wa Mikono kwa Walemavu wa Usikivu 2023 huko Copenhagen na Michezo ya Dunia ya Vijana kwa Walemavu wa Usikivu 2024 huko Sao Paulo.

Kwa sasa, timu ya wanaume ya Kenya inashikilia nafasi ya 12 duniani, huku timu ya wanawake ikiwa nafasi ya 9. Kwa majaribio yanayoendelea, matarajio ni makubwa kwamba kikosi cha mwisho kitakuwa cha ushindani katika jukwaa la dunia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending