Sports
Mo Salah Aibuka Mchezaji Bora wa PFA kwa Mara ya Tatu, Baada Ya Kuiongoza Liverpool Kutwaa Taji
Mahambulizi wa Liverpool Mohamed Salah ametangazwa Mchezaji Bora wa Wachezaji wa PFA (PFA Players’ Player of the Year) baada ya msimu wa kihistoria wa 2024-25 ambapo alishinda taji la ligi na Liverpool, akifunga mabao 29 na kushinda kiatu cha dhahabu (Golden Boot) kwa mara ya nne.
Idadi yake ya juu zaidi ya pasi za mabao msimu uliopita, 18, ni rekodi bora zaidi katika historia ya Premier League ikizidiwa tu na Kevin de Bruyne na Thierry Henry.
Mwanasoka huyo kutoka Misri pia amekuwa mchezaji wa kwanza kabisa kushinda tuzo hiyo mara tatu, na vilevile ameorodheshwa kwenye Kikosi cha Mwaka cha Premier League akiwa na wachezaji wenzake watatu – Virgil van Dijk, Ryan Gravenberch na Alexis Mac Allister.
Salah alipokea tuzo hiyo mikononi mwa Ian Rush, mfungaji bora wa muda wote wa Liverpool. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 alishinda kura mbele ya Mac Allister, Bruno Fernandes, Alexander Isak, Cole Palmer na Declan Rice.
Katika kikosi bora cha msimu wa mwaka msimu jana;
Matz Sels (Nottingham Forest)
William Saliba (Arsenal)
Gabriel (Arsenal)
Virgil van Dijk (Liverpool)
Milos Kerkez (Bournemouth, now Liverpool)
Declan Rice (Arsenal)
Alexis Mac Allister (Liverpool)
Ryan Gravenberch (Liverpool)
Mohamed Salah (Liverpool)
Chris Wood (Nottingham Forest)
Alexander Isak (Newcastle)
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

