Connect with us

Sports

Morocco Yaandika Historia kwa Kutwaa Taji la CHAN 2024 Baada ya Kuibwaga Madagascar 3-2

Published

on

Timu ya Taifa la Morocco Atlas Lions imejikita zaidi katika historia ya soka barani Afrika baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Madagascar kwenye fainali ya michuano ya African Nations Championship (CHAN) 2024 iliyopigwa Jumamosi jioni katika Uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani.

Atlas Lions, waliokuwa tayari mabingwa mara mbili, walionesha ustahimilivu na ubora wa kiwango cha juu na kuwa taifa la kwanza kutwaa taji la CHAN mara tatu.

Ushindi huo ulipatikana ndani ya dakika 90, mbele ya mashabiki walioujaza uwanja, na kukamilisha mashindano ya Pamoja CHAN 2024 yaliyodumu kwa mwezi mzima kwa mtindo wa kusisimua.

Madagascar, waliokuwa wakisaka taji lao la kwanza barani, waliwashangaza Wamorocco mapema kipindi cha kwanza baada ya Clavin Felicite Mantanosoa kufunga bao safi la nusu-voli, akipokea pasi kutoka kwa Nantenaina Razafimahatana.

Hata hivyo, Morocco hawakutetereka. Mshambuliaji Youssef Mehri alisawazisha kupitia kichwa kizuri akimalizia krosi ya kupinda ya Khalid Baba.

Kabla ya mapumziko, Morocco walipiga tena. Mfungaji bora wa mashindano, Oussama Lamlioui, alifunga sekunde za mwisho za kipindi cha kwanza na kuwapa Waarabu wa Kaskazini uongozi wa mabao 2-1.

Kocha wa Madagascar, Romuald Rakotondraibe, alifanya mabadiliko matatu mwanzoni mwa kipindi cha pili yaliyoinua kasi ya kikosi chake. Hatua hiyo ilizaa matunda dakika ya 68 wakati T.N Rakotondraibe aliposawazisha mabao 2-2, na kupelekea shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki wao.

Lakini ubora wa Morocco uliwashinda wapinzani wao. Zikiwa zimesalia dakika 10 pekee kabla ya filimbi ya mwisho, Lamlioui alitoa burudani ya kipekee kwa kufumua kombora kali kutoka mbali na kufunga bao la ushindi, huku akimalizia kampeni yake kwa mabao saba na kuibuka mfungaji bora.

Ushindi huo haukuwapa Morocco tu taji bali pia kitita cha KSh milioni 455. Atlas Lions sasa wamesimama peke yao kama taifa pekee kutwaa taji la CHAN mara tatu, baada ya kulitwaa mwaka 2018 nyumbani, tena mwaka 2020, kabla ya kukosa toleo la 2023.

Katika safari yao kuelekea taji, Morocco waliwaondoa mabingwa watetezi Senegal kwa mikwaju ya penalti kwenye nusu fainali.

Kwa upande wao, Madagascar walipata heshima kubwa baada ya safari ya kuvutia iliyojumuisha kuwatoa wenyeji Kenya na Sudan. Kadri pazia la CHAN 2024 linaposhuka, macho sasa yameelekezwa kwenye AFCON 2027 ambayo Kenya, Uganda na Tanzania wataandaa kwa pamoja, ikiashiria onyesho lingine kubwa kwa mashabiki wa soka barani Afrika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending