Connect with us

Entertainment

Msanii Sammy Kioko Aweka Gari Lake Sokoni Ili Kugharamia Matibabu ya Dada Yake

Published

on

Mchekeshaji maarufu wa Kenya, Sammy Kioko, ametangaza kuwa ameamua kuuza gari lake ili kukusanya fedha za kugharamia matibabu ya dada yake ambaye anapitia changamoto kubwa kiafya.

Kupitia chapisho lake aliloweka kwenye Instagram Stories, Kioko alieleza jinsi uamuzi huo ulivyokuwa mgumu kwake, lakini ni hatua aliyoilazimika kuchukua kwa ajili ya familia yake.

“Asanteni kwa simu, maombi na maneno ya faraja. Kwa wanaonijua, hii gari imekuwa baraka yangu kwa miaka minane. Wale ambao wamekuwa wakinifuatilia kwa miaka kumi wanajua nilivyopata gari hili. Wakati mwingine, kama mwanaume, lazima ufanye kile kinachopaswa kufanyika hata kama kinauma,” aliandika.

Akiendelea kueleza, Kioko alisema kuwa hataki kusema kuwa “anauza gari”, bali anataka kubariki mtu nalo kwa bei nzuri.”

“Mwezi huu wa Novemba nilikuwa nimepanga kumsafirisha dada yangu kwenda kutafuta matibabu. Hata hivyo, muda si rafiki wetu,” aliongeza kwa huzuni.

Kioko, ambaye amekuwa akijulikana kwa ucheshi wake katika jukwaa la Churchill Show na kazi zake za mtandaoni, amepokea wimbi la faraja na sala kutoka kwa mashabiki na marafiki mitandaoni.

Wengi wamemsifu kwa moyo wake wa kujitolea na upendo wa kifamilia, wakimtakia dada yake afya njema na uponyaji wa haraka.

Chapisho hilo limekuja siku chache baada ya Sammy Kioko kushiriki picha kwenye ukurasa wake wa Facebook, ikimuonesha dada yake akiwa hospitalini akipokea matibabu.

Katika maelezo yaliyofuatana na picha hiyo, Kioko alionyesha kukatishwa tamaa kutokana na kucheleweshwa kwa malipo ya mradi ambao anadai aliukamilisha kwa Serikali ya Kaunti ya Machakos — fedha ambazo amesema ni muhimu kugharamia matibabu ya dada yake yanayoendelea.

“Ukiamua kunyamaza katika hali ya dhuluma, basi umechagua upande wa mnyanyasaji! Hakuna mtu anaomba misaada ya bure — ni malipo ya kazi iliyofanywa. Hiyo ilikuwa upasuaji wake wa kwanza. Tumekuwa tukirudi hospitalini kwa ukaguzi wa kawaida, tukingoja na kuomba tulipwe angalau kugharamia upasuaji wa pili unaotakiwa kufanyika,” aliandika.

Kioko aliendelea kuiomba serikali ya kaunti kuweka utu mbele kuliko siasa, akidai kwamba jitihada za familia yake za kuomba msaada zimegeuzwa suala la kisiasa.

“Serikali ya kaunti, tuweke utu mbele — si kila kitu kiingizwe kwenye siasa! Tuliomba msaada, lakini tukageuzwa mazungumzo ya kisiasa. Hii si haki. Tunachohitaji ni malipo yetu tu,” aliongeza kwa hisia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Mimi Ndo Msanii Nimebaki Wengine ni Content Creators! – Hubby Africana

Published

on

Msanii wa nyimbo za kizazi kipya, Hubby Africana, ameibua mjadala mpana mitandaoni baada ya kauli yake ya hivi karibuni aliyochapisha kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Kupitia ujumbe huo, Hubby Africana alijinasibu kuwa yeye ndiye msanii halisi aliyebaki katika tasnia, akiwatuhumu wengine kwa kugeukia zaidi uundaji wa maudhui badala ya muziki.

Aliandika kwa kujiamini: “Mimi ndo msanii nimebaki🤔 hao wengine wamekua content creator😂😂 very soon mtanielewa #mnyama is coming stay tuned 🔥💯.”

Hubby Africana si jina geni kabisa pwani. Msanii huyo alishiriki kwenye makala ya kwanza ya Kilifi All Stars 2025, ambapo aliweza kumaliza katika nafasi ya saba kwa kupata kura 258. Ushiriki wake kwenye shindano hilo ulimuweka karibu zaidi na mashabiki na kumpa jukwaa la kuonesha kipaji chake.

Katika shindano hilo, aliingia na wimbo wake unaojulikana kama “Ndakukunda”, ambao ulimtambulisha rasmi kwa hadhira pana zaidi. Wimbo huo ulionyesha uwezo wake katika kuunganisha ladha ya muziki wa mapenzi na vionjo vya kisasa vinavyovutia kizazi cha sasa.

Kauli yake ya hivi karibuni inaonekana pia kuwa sehemu ya mkakati wa kujitangaza, hasa kwa kuzingatia alivyotumia kauli “#mnyama is coming.”

Je, Hubby analenga kujitofautisha na wengine na kujiweka katika daraja la kipekee? Swali kubwa linalobaki ni kama ataweza kusimama imara na kuthibitisha madai yake kupitia ubora wa kazi zake zijazo. Katika ulimwengu wa muziki, ushindani ni mkali—na mwisho wa yote, muziki mzuri ndio unaozungumza zaidi kuliko maneno. Tusubiri.

Continue Reading

Entertainment

Live Yageuka Vita: Beka Ruga Amvaa Madundo Bila Huruma

Published

on

Mtengeneza maudhui maarufu Beka Ruga amezua mjadala mkali mitandaoni baada ya kumkosoa vikali mchekeshaji Madundo wakati wa “live” aliyofanya pamoja na Bujra saa chache zilizopita.

Akijibu swali la kwa nini hajawahi kushirikiana na Madundo, Ruga hakuficha hisia zake. Alisema wazi kuwa haoni aina ya content ambayo wanaweza kufanya pamoja, akimtaja Madundo kama mtu anayependelea kuvaa nguo chafu na kukimbia mitaani kama sehemu ya burudani yake.

Kauli hiyo haikuishia hapo. Ruga aliendelea kusema kuwa kama angepewa nafasi ya kumbadilisha Madundo, angeanza kwa kumshauri aache kujipaka makaa na aanze kuzingatia usafi wake binafsi. Kwa mujibu wa Ruga, kujipaka makaa kunaweza kuwa na madhara kiafya, akihusisha hata hatari ya saratani.

Aidha, alimkosoa pia kwa kile alichokiita “kujidhalilisha” alipokuwa Tanzania, akidai kuwa Madundo alipiga picha na Gigy Money akiwa amevaa mavazi yasiyofaa hadharani.

Hata hivyo, licha ya ukosoaji huo mkali, Ruga alikanusha kuwa na bifu na Madundo. Alisema wote wanatoka eneo moja (Mkwale) na wana uwezo wa kufanya kazi nzuri pamoja—lakini akasisitiza kuwa Madundo anahitaji kubadilika ili kueleweka zaidi kwenye tasnia.

Sasa swali linabaki: je, huu ni ushauri wa kujenga au ni mashambulizi yaliyovuka mipaka?

Kwa upande mmoja, baadhi ya watu wanaona Ruga kama mtu anayesema ukweli ambao wengi wanaogopa kuusema. Kwa mwingine, wapo wanaoamini kuwa kila msanii ana mtindo wake wa kipekee, na kile kinachoonekana “cha ajabu” kwa mmoja, ndicho kinachomtofautisha na kumuinua mwingine.

Katika ulimwengu wa uundaji maudhui creation, utofauti ndio nguvu. Lakini pia, taswira na namna mtu anavyojiwasilisha vinaweza kuathiri namna anavyopokelewa na fursa anazopata.

Wewe unaonaje—Beka Ruga yuko sahihi au amevuka mipaka?

Continue Reading

Trending