Connect with us

Sports

Mshambulizi Erling Haaland afunga mara mbili huku Manchester City wakiizamisha Manchester United debi la Manchester

Published

on

Mshambulizi Erling Haaland alifunga mabao mawili huku Manchester City ikiipa pigo jingine Manchester United ya kocha Ruben Amorim kwa ushindi wa 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu Jumapili.

Kiungo wa Uingereza Phil Foden alifungua ukurasa wa mabao kabla Haaland hajachukua usukani kipindi cha pili kwa mabao mawili, licha ya kukosa nafasi ya ajabu katikati ya magoli hayo, huku City ikirejea kwenye ushindani baada ya kupoteza michezo miwili mfululizo ya ligi.

United waliingia kwenye derby wakiwa juu ya City kwenye msimamo kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitano. Hata hivyo, hilo lilitokana zaidi na udhaifu wa City mwanzoni mwa msimu kuliko maendeleo ya kikosi cha Amorim, ambacho kimekusanya alama nne pekee katika mechi nne za kwanza na kutolewa kwenye Carabao Cup na Grimsby ya daraja la nne.

Kipa mpya Gianluigi Donnarumma alihitimisha onyesho bora la City kwa kuokoa shuti kali la Bryan Mbeumo na kuwanyima United nafasi ya kurejea mchezoni wakiwa nyuma 2-0.

City wamesalia nyuma kwa pointi sita dhidi ya vinara Liverpool, lakini ushindi huu unawapa morali kubwa kabla ya michezo migumu dhidi ya mabingwa wa Serie A Napoli na wapinzani wa ubingwa wa EPL Arsenal wiki ijayo.

Kabla ya mechi, mashabiki wote waliweka kando uhasama na kumpa heshima bingwa wa ndondi Ricky Hatton, shabiki mkubwa wa City, aliyefariki Jumapili akiwa na miaka 46. Uso wake ulionyeshwa kwenye skrini kubwa wakati wa dakika moja ya makofi.

Foden, ambaye pia ni shabiki wa utotoni wa City, alisema habari hizo ziliwapa wachezaji motisha ya ziada kushinda kwa heshima ya Hatton. Na kweli, Mwingereza huyo alikuwa mhimili wa ushindi muhimu baada ya kuanza msimu vibaya.

Mchezaji huyo bora wa EPL msimu wa 2023/24 alikuwa akipitia wakati mgumu msimu uliopita, akipoteza kiwango chake. Masuala ya kiafya yalimsababisha kutoanza mechi yoyote msimu huu hadi Jumapili, lakini alichukua dakika 18 pekee kuonyesha makali yake.

Ulinzi wa United uliporuhusu Jeremy Doku kupenya na kutoa krosi iliyo mkuta Foden akiwa hana ulinzi, naye akafunga kwa kichwa.

Kocha Amorim aliamua kuendelea kumpa nafasi kipa Altay Bayindir badala ya sajili mpya Senne Lammens, lakini haikusaidia.

Donnarumma waamua

Tijjani Reijnders alifyatua shuti moja kwa moja kwa Bayindir badala ya kuipa City bao la pili mapema, lakini Doku alihusika tena dakika ya 53 wakati Haaland alipoonyesha nguvu, kasi na umakini kwa kumchungulia Bayindir na kufunga bao la pili.

Haaland alipoteza nafasi rahisi muda mfupi baadaye baada ya kupokea pasi nzuri kufuatia makosa ya Matthijs de Ligt. Akiwa amemzunguka Bayindir, aligonga mwamba badala ya kufunga.

Muda mfupi baadaye, Donnarumma aliokoa kwa kishindo shuti la Mbeumo lililokuwa linaelekea kona ya chini, jambo lililozuia United kurejea mchezoni.

Badala ya 2-1, matokeo yakawa 3-0 baada ya Harry Maguire kumpoteza mpira kwa urahisi na Bernardo Silva kumpasia Haaland, ambaye alikimbia nusu uwanja wa United na kufunga kwa utulivu.

Hilo lilikuwa bao lake la nane katika mechi tisa dhidi ya United.

Reijnders alikosa kuongeza maumivu ya United baada ya kupiga nje akiwa na nafasi nzuri ya uso kwa uso na Bayindir.

Mashabiki wa City walimshangilia Amorim kwa nyimbo za “Sacked in the morning” (anafutwa asubuhi).

Ingawa haipo hatarini kufutwa mara moja, rekodi ya Amorim kwenye EPL sasa ni mbaya: ushindi 8 pekee katika mechi 31

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending