Sports
Nataka Stars Kwenye Fainali Ya Chan Asema Mvurya
Waziri wa Michezo Salim Mvurya amesema kwamba lengo lake ni kuona timu ya Soka Harambee Stars katika fainali ya kombe la CHAN linalongoa nanga mwezi ujao hapa nchini.
Akizungumza na wanahabari Mvurya amesema kwamba miondo misingi iko tayari na wanaipa timu ya soka kila kitu kufanya vyema katika mashindano hayo yanayoandaliwa kwa mara ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki Kenya,Uganda na Tanzania.
“Kwa sasa naweza nikathibitishia Wakenya tuko vizuri kwa kombe la CHAN,kuna wakati timu zetu zimkeua zikitatizika mpaka kucheza mechi za kufuzu nje ya nchi kwani hatukua na uwanja wa kutumia ila sasa ni furaha kuwa na viwanja vya viwango kama Kasarani na Nyayo.”
Waziri huyo ameongezea kwamba kwa sasa Stars ina kocha mwenye tajriba na serikali kupitia kwa Wizara yake itaipa sapoti kocha huyo kuleta matokeo chanya.
Kwa mujibu wa Mvurya itakua vyema zaidi Stars wakifika Fainali ambayo inachezwa ugani Kasarani Agosti 30.
“Lengo letu ni kuona Stars kwenye Fainali maanake itakua bora zaidi fainali inaypigwa Kasarani,mashabiki wajitokezee tusapoti vijana wa nyumbani.”
Stars wanafungua kampeini yao dhidi ya DR.Congo Agosti 3 ugani Kasarani.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

