Connect with us

Published

on

Aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Tume ya umoja wa Afrika, AUC, kutoka Kenya, Raila Odinga, amevunja kimya chake na kuzungumzia uchanguzi wa nafasi hiyo uliyofanyika siku ya Jumamosi.

Akihutubia wajumbe wakenya akiwa jijini Addis Ababa nchini Ethiopia, Odinga amesema wakenya wanafaa kusitisha uvumi kwamba alishindwa kutokana na uzee, ama kukosa kufanya kampeni bora.

Odinga amesema kuna maswala muhimu ambayo yanafaa kuangaziwa ili changuzi zijazo iwe rahisi kwa Kenya kunyakua kiti hicho na wala sio kwa wakenya kuendeleza propaganda zisizo na manufaa yoyote.

Odinga hata hivyo amempogeza rais William Ruto kwa kuhakikisha kampeni zake zinafanyika vyema sawa na kumpangia vikao na marais wa mataifa ya Afrika ili kutafuta uugwaji mkono, japo hakufaulu.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Trump asema Marekani itasitisha vita dhidi ya Iran

Published

on

By

Rais Donald Trump amesema kwamba Marekani itaondoka Iran hivi karibuni na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.

Rais Trump alisema Marekani imefikia malengo iliyojiwekea kabla ya kuanza kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Iran mwezi uliyopita kwa ushirikiano na Israel.

Aidha aliongeza kuwa lengo la kuizuia Iran kuwa na uwezo wa kuunda silaha za nyuklia limefikiwa na sasa Marekani inamaliza kazi.

Trump pia aliema Marekani sasa inatawala anga za Iran na pia imepata mabadiliko ya utawala kufuatia mauaji ya viongozi wakuu wa kisiasa na kijeshi.

Aliwataja viongozi hao wapya mjini Tehran kama walio na misimamo mikali na waadilifu zaidi, ikilinganishwa na watangulizi wao.

Trump pia alisema viongozi wa Iran wanaomba kufanya makubaliano na Marekani ili kumaliza vita, madai ambayo hapo awali yalipingwa na Iran na kuongeza kwamba vita vinaweza kumalizika bila makubaliano kati ya pande hizo mbili.

Kuhusu athari za vita hasa kupanda kwa bei ya mafuta, rais Trump alisema bei itashuka mara tu Marekani itakapomaliza hatua zake za kijeshi.

Continue Reading

International News

Bunge la Israel limepitisha sheria mpya ya adhabu ya kifo

Published

on

By

Bunge la Israel limepitisha sheria mpya inayotoa adhabu ya kifo kwa Wapalestina watakaopatikana na hatia ya mashambulizi ya mauaji dhidi ya Waisrael.

Sheria hiyo ilipitishwa kwa kura 62 dhidi ya 48, huku mbunge mmoja akijizuia kupiga kura na wengine kutohudhuria kikao hicho.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alihudhuria kikao hicho na kupiga kura kuunga mkono mswada huo bungeni.

Mswada huo wa sheria uliwasilishwa na Waziri wa usalama wa taifa hilo Itamar Ben Gvir, ambaye ni mmoja wa wanasiasa wenye msimamo mkali nchini humo.

Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa wa kimataifa, huku mataifa ya Umoja wa Ulaya na mashirika ya haki za binadamu yakielezea wasiwasi mkubwa.

Muda mfupi baada ya kupitishwa, kundi la haki za binadamu la Israel lilisema limewasilisha malalamiko katika Mahakama kuu ya nchi hiyo.

Mamlaka ya Palestina ilitaja mswada huo kama uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Palestina, ikisema kwamba unakiuka mkataba wa Geneva.

Hata hivyo mamlaka ya Washington ilisema kwamba Israel ina haki ya kutungu sheria zake huku nchi zikiwemo Ujerumani, Ufaransa, Italia na Uingereza zikielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mswada huo.

Continue Reading

Trending