Sports
Noni Madueke Atua Arsenal
Sasa ni Rasmi Noni Madueke ni mali ya Arsenal vilabu vyote viwili vimekubaliana kwa ajili ya uhamisho huo wa pauni milioni 52 dhidi ya Muingereza huyo.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuwasili mjini London kwa ajili ya vipimo vya kiafya kabila ya kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na wanabunduki hao wa London Kaskazini.
Madueke mwenye umri wa miaka 23 anakua sajili wa nne kwa kocha Mikel Arteta baada ya kuwasili kwa kipa Kepa Arrizabalaga, kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi na kiungo Christian Norgaard kutoka Brenford.
Nyota huyo amekua na kilabu ya The Blues nchini Marekani kwa kombe la Dunia baina ya vilabu huku akiacha kilabu yake ikijianda kwa fainali Jumapili hii.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

