Sports
Omanyala Aikosa Fainali ya Diamond League 2025 Kwa Sababu za Majeraha
Mwanariadha wa kasi zaidi barani Afrika, Mkenya Ferdinand Omanyala, amethibitisha kwamba hatashiriki kwenye Fainali ya Diamond League ya 2025 kutokana na changamoto za majeraha.
Nyota huyo wa mbio fupi, ambaye ni bingwa wa Afrika mara mbili na mshindi wa dhahabu wa mita 100 kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola, alitoa tangazo hilo kupitia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii.
Omanyala alifichua kwamba amekuwa akikumbwa na maumivu ya kudumu kwenye nyonga, misuli ya iliopsoas na sehemu ya gluteal kwa wiki kadhaa zilizopita, hali ambayo imevuruga maandalizi yake kwa ajili ya mashindano hayo makubwa.
Alisema kwamba usumbufu huo umeathiri uwezo wake wa kushindana kwa kiwango cha juu, na hivyo kumlazimu kujiondoa kwenye Fainali ya Diamond League iliyopangwa kufanyika Agosti 27–28 mjini Zurich, Uswizi.
“Kwa sababu ya maumivu ya hivi karibuni kwenye nyonga, misuli ya iliopsoas na gluteal katika wiki chache zilizopita, nasikitika kuwataarifu kuwa sitaweza kushiriki kwenye Fainali ya Diamond League ya 2025,” aliandika Omanyala.
Hata hivyo, licha ya pigo hilo, nyota huyo wa mbio fupi ameendelea kuwa na matumaini ya kurejea kwa nguvu.
Ameeleza kujiamini kwamba atapona kwa wakati muafaka ili kuiwakilisha Kenya kwenye Mashindano ya Dunia ya Riadha yatakayofanyika Tokyo, Japani kuanzia Septemba 13 hadi 21.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

