Connect with us

Sports

Oscar Piastri Aibuka Bingwa Katika Mashindano ya Dutch Formula One Grand Prix

Published

on

Mwendeshaji wa magari dereva Oscar Piastri kutoka Australia alitumia nguvu na ustadi kushinda mbio zenye matukio mengi za Dutch Formula One Grand Prix hapo jana, huku kipenzi cha mashabiki wa nyumbani, Max Verstappen, akimaliza nafasi ya pili na Lando Norris wa McLaren mwenzake wa Piastri akipata hitilafu kubwa dakika za mwisho za mbio.

Piastri aliongoza kuanzia nafasi ya kwanza hadi mwishoni katika uwanja wa Zandvoort, mbio ambazo gari la usalama liliingia mara kadhaa, hali iliyomsaidia kuimarisha uongozi wake dhidi ya Norris kwa alama 34 kwenye msimamo wa ubingwa.

Kinda wa Kifaransa mwenye umri wa miaka 20 kutoka Racing Bulls, Isack Hadjar, alimaliza nafasi ya tatu na kuwa dereva wa tano mdogo zaidi kuwahi kufika kwenye jukwaa la ushindi. Hii ilikuwa ni ushindi wa sita wa Grand Prix kwa Piastri msimu huu, ukithibitisha hadhi yake kama dereva wa kuwindwa kwenye mbio za ubingwa wa madereva mwaka huu.

Mbio zilianza kwa msisimko mkubwa ambapo Verstappen, aliyeanza nafasi ya tatu, alimzidi Norris lakini kisha akapoteza udhibiti wa Red Bull yake kwa muda mfupi.

Hata hivyo, akishangiliwa na maelfu ya mashabiki wake waliovalia rangi ya chungwa (“Orange Army”), Verstappen alirejea kwa ustadi na kujipanga nyuma ya Piastri, aliyekuwa ameanza vizuri.

Lakini mwendo wa kasi wa magari ya McLaren ulidhihirika haraka, na Norris akampita Mholanzi huyo upande wa kushoto kwenye raundi ya tisa, kurejesha nafasi ya kwanza na ya pili kwa timu ya papaya.

Kitu kisichojulikana kabla ya mbio kilikuwa hali ya hewa kwenye uwanja maarufu kwa kubadilika ghafla, ulio karibu na pwani ya Bahari ya Kaskazini. Mvua ya kwanza ilinyesha karibu na raundi ya 15 kati ya 72, na baada ya raundi kumi tu ikawaathiri, huku bingwa mara saba wa dunia, Lewis Hamilton, akiteleza na Ferrari yake kutoka barabarani na kugonga vizuizi.

“Samahani sana jamani,” alisema Hamilton, ambaye hakujeruhiwa, lakini kwenye Grand Prix iliyopita alikuwa amejieleza kama dereva “asiye na maana kabisa” ambaye anapaswa kubadilishwa.

Gari la usalama liliporudi tena barabarani, uwanja wa magari ulipungua tofauti lakini Piastri aliendelea kumkabili Norris, ambaye naye alimzuia Verstappen aliyekuwa akishikilia nafasi ya tatu.

Nyuma ya vinara hao, dereva wa Ferrari, Charles Leclerc, alionyesha ujasiri wa hali ya juu kwa kumpita George Russell wa Mercedes kwa mbinu ya kipekee ya ku-overtake.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending