Sports
PSG Imepunguza Ada ya Ununuzi wa Kipa Gianluigi Donnarumma
Kilabu ya PSG ya Ufaransa imeripotiwa kupunguza ada waliyotarajia kwa kipa wa Kiitaliano Gianluigi Donnarumma kufuatia nia kutoka kwa kilabu ya Manchester City.
Donnarumma, mwenye umri wa miaka 26, ameuhusishwa na Citizens, ambao wanatafuta kipa mpya iwapo Ederson ataondoka klabuni.
Kulingana na RMC Sport, mabingwa wa sasa wa Ligi ya Mabingwa wamepunguza bei yao kutoka pauni milioni 43 hadi kati ya pauni milioni 26 na 30, ikizingatiwa kuwa Donnarumma amebakisha mwaka mmoja pekee kwenye mkataba wake jijini Paris.
Hali hiyo imemfanya Luis Enrique kuachana na mchezaji muhimu wa kikosi chake kilichoshinda Ligi ya Mabingwa, na kumweka badala yake Lucas Chevalier.
Nguli wa taarifa za Uhamisho Fabrizio Romano pia ameripoti kuwa masharti binafsi yamekubaliwa kati ya Donnarumma na Manchester City, huku dili hilo likionekana kukaribia kukamilika.
Kuingia kwa Donnarumma kungehitaji kuzingatiwa kwa kuuzwa kipa namba moja wa muda mrefu wa Guardiola, Ederson. Mbrazil huyo, ambaye amechezea klabu hiyo tangu mwaka 2017, hakudumu kama chaguo la kwanza msimu uliopita, mara nyingi akibadilishana nafasi na Stefan Ortega.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

