Sports
Rwanda yaandika historia: Taifa la kwanza Afrika kushirikiana na NBA na NFL kwa udhamini wa utalii
Rwanda yatangaza udhamini wa muda mrefu na Los Angeles Rams na LA Clippers, na kuwa taifa la kwanza barani Afrika kushirikiana na NFL na NBA kwa ajili ya utalii.
Nembo ya utalii Visit Rwanda, inayoendeshwa na Bodi ya Maendeleo ya Rwanda (RDB), itaonekana kama mdhamini rasmi wa kiraka cha jezi cha LA Clippers, huku uwanja wa nyumbani wa Los Angeles Rams pia ukibeba chapa hiyo.
“Ushirikiano huu unatuwezesha kupeleka uzuri wa kipekee wa asili ya Rwanda na bioanuwai yake ya ajabu kwa watu wa Los Angeles pamoja na mashabiki wa NBA na NFL kote duniani,” alisema Jean-Guy Afrika, Mkurugenzi Mkuu wa RDB katika taarifa yake.
Nchi hiyo ya Afrika Mashariki imekuwa ikijitangaza kwa muda mrefu kama kitovu cha matukio makubwa ya michezo na kinara wa utalii wa ikolojia — ikiwa ni sehemu ya jitihada zake kuvutia wawekezaji na kuondoka kwenye kivuli cha mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.
Mnamo 2018, Rwanda ilikua mdhamini rasmi wa klabu ya soka ya Uingereza, Arsenal FC, ambapo nembo ya “Visit Rwanda” iliwekwa kwenye mikono ya jezi za wachezaji.
Kigali pia imeingia mikataba na vilabu vingine vya mpira wa miguu kama Paris Saint-Germain (PSG) na kwa sasa inapigania kuwa mwenyeji wa mashindano ya Formula One.
Wiki iliyopita, Rwanda pia iliandika historia kwa kuwa taifa la kwanza barani Afrika kuandaa mashindano ya dunia ya mbio za baiskeli, yaliyokamilika Jumapili.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

