Connect with us

Sports

Sare Tasa na Burkina Faso Yaahirisha Ndoto za Misri Kufuzu Kombe la Dunia

Published

on

Matumaini ya taifa la Misri la kufuzu Kombe la Duniabado  baada ya kutoka sare tasa ya 0-0 dhidi ya Burkina Faso kwenye mechi ya Kundi A iliyochezwa Ouagadougou, Jumanne.

Kikosi cha Hossam Hassan ambacho hakijapoteza mchezo wowote kimefikisha pointi 20 na kuongoza Kundi A kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Burkina Faso, huku kukiwa na mechi mbili pekee zikisalia kwenye mchujo.

Kwa kuwa ni washindi wa makundi pekee wanaofuzu moja kwa moja, mabingwa wa Afrika mara saba wanahitaji alama mbili pekee kutoka kwa michezo yao miwili ya mwisho ili kujihakikishia nafasi na kufanikisha ushiriki wao wa nne kwenye Kombe la Dunia. Watakutana na Djibouti na Guinea-Bissau mwezi Oktoba.

Kocha wa Misri, Hassan, hata hivyo, alisherehekea matokeo hayo ambayo yamewasogeza hatua moja karibu na kufuzu katika mashindano makubwa ya timu 48 yatakayofanyika Amerika Kaskazini mwaka ujao.

“Ni siku kubwa kwa watu wa Misri… Ningependa kuwashukuru kila mchezaji kwa juhudi zao dhidi ya timu ngumu ambayo ina wachezaji wanaocheza Premier League, Bundesliga na Ligue 1,” alisema Hassan, mshambuliaji wa zamani wa Misri aliyewaongoza kufuzu Kombe la Dunia mwaka 1990, akizungumza na kituo cha On Sport.

“Licha ya kucheza ugenini Burkina Faso, tulicheza kwa mtindo chanya na kuunda nafasi kubwa. Wakati huohuo, tulidumisha uwiano. Tungelikuwa tumefunga goli moja au mawili kabla ya mwisho,” aliongeza.

Misri ilipata pigo mapema baada ya mshambuliaji wa Manchester City, Omar Marmoush, kulazimika kutoka nje kwa majeraha dakika ya 9.

Fursa yao bora ilikuja dakika ya 67 wakati Mohamed Salah alipompasia Osama Faisal lakini shuti lake likakataliwa kwa kuotea. Trezeguet wa Misri alikosa nafasi ya kwanza ya mchezo baada ya jaribio lake kuokolewa na kipa wa Burkina Faso, Herve Koffi.

Wenyeji hawakuwa na mashambulizi mengi, huku mshambuliaji wa Sunderland, Bertrand Traore, akiongoza juhudi zao bora.

Misri walikaribia kufunga goli la ushindi dakika za mwisho, lakini Mostafa Mohamed alipoteza nafasi mbili muhimu.

Hassan, ambaye ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Misri, anatarajiwa kuwa wa kwanza kuongoza taifa hilo kufika Kombe la Dunia akiwa mchezaji na pia kocha.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 alisema: “Lengo langu lilikuwa kufundisha timu ya taifa ya Misri. Nimekuwa nikiota kila mara jambo hilo. Nataka kutimiza ndoto ya mashabiki na kuishi kwa imani yao (kwa kuongoza timu kufuzu Kombe la Dunia).”

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending