Sports
Serani Waahidi Kutetea Ubingwa Mashindano Ya Shule ya Upili
Mabingwa watetezi wa soka kwa shule za upili kaunti ya Mombasa upande wa wavulana, shule ya upili ya SERANI walianza vyema kampeni ya kutetea taji lao kwa kupata ushindi katika mechi zao zote za makundi.
Katika mechi ya kwanza waliicharaza shule ya upili ya Kajembe 3-0 na Kisha wakawageukia vijana wa shule ya upili ya Khadija na kuwalaza mabao 2-0.Katika mechi zingine, St Charles Lwanga wameona moto kwa kutandikwa 1-0 na Tononoka, Kisha Khadija wakavuna ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Shikaadabu, Moi Forces Academy wakiwachapa St Charles Lwanga 2-0 na Kajembe wakatoka 1-2 dhidi ya Shikaadabu.
Shule ya upili ya Mwakirunge bahati haikuwa upande wao kwani baada ya kupokea kichapo cha mabao 5-0 kutoka kwa Moi Forces katika mechi ya kwanza, hawakuweza kurejea uwanjani kwa kipindi cha pili cha mechi yao ya pili dhidi ya Tononoka ambapo tayari walikuwa wamechapwa magoli 3-0 katika kipindi cha kwanza, wakieleza kuwa hatua hiyo imetokana na wachezaji wengi kupata majeraha wakiwa uwanjani na kubaki na wachezaji 6 pekee.
MOMBASA COUNTY KSSSA DAY 2 FIXTURES
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

