Sports
Serani Waahidi Kutetea Ubingwa Mashindano Ya Shule ya Upili
Mabingwa watetezi wa soka kwa shule za upili kaunti ya Mombasa upande wa wavulana, shule ya upili ya SERANI walianza vyema kampeni ya kutetea taji lao kwa kupata ushindi katika mechi zao zote za makundi.
Katika mechi ya kwanza waliicharaza shule ya upili ya Kajembe 3-0 na Kisha wakawageukia vijana wa shule ya upili ya Khadija na kuwalaza mabao 2-0.Katika mechi zingine, St Charles Lwanga wameona moto kwa kutandikwa 1-0 na Tononoka, Kisha Khadija wakavuna ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Shikaadabu, Moi Forces Academy wakiwachapa St Charles Lwanga 2-0 na Kajembe wakatoka 1-2 dhidi ya Shikaadabu.
Shule ya upili ya Mwakirunge bahati haikuwa upande wao kwani baada ya kupokea kichapo cha mabao 5-0 kutoka kwa Moi Forces katika mechi ya kwanza, hawakuweza kurejea uwanjani kwa kipindi cha pili cha mechi yao ya pili dhidi ya Tononoka ambapo tayari walikuwa wamechapwa magoli 3-0 katika kipindi cha kwanza, wakieleza kuwa hatua hiyo imetokana na wachezaji wengi kupata majeraha wakiwa uwanjani na kubaki na wachezaji 6 pekee.
MOMBASA COUNTY KSSSA DAY 2 FIXTURES
Entertainment
Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy
Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.
Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.
Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.
“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.
Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.
Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.
Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.
Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

