Connect with us

News

Wakaazi watishia kuandamana kufuatia uhaba wa maji Kilifi

Published

on

Wakaazi wa kaunti ya Kilifi wametishia kuandamana hadi katika ofisi za Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro kufuatia uhaba maji uliyodumu kwa takribani mwezi mmoja katika baadhi ya maeneo ya kaunti hiyo.

Wakaazi hao wakiongozwa na Kiongozi wa kidini wa Kanisa la Kibaptist kanda ya Pwani Rev. Francis Katana, walisema suala la maji ni muhimu kwa jamii za kaunti ya Kilifi na kwamba serikali ya kaunti inafaa kulichukuliwa kwa uzito suala hilo na kulitatua.

Katana anasema idadi kubwa ya wakaazi hasa wa mji wa Malindi wamekuwa wakipitia changamoto hiyo kwa mda mrefu na hata baada ya kuwasilisha lalama zao kwa idara husika ikiwemo ofisi za Kampuni ya usambazaji maji ya Malindi, MAWASCO, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kukabiliana na changamoto hiyo.

Kiongozi huyo wa kidini alisisitiza kwamba maandamano hayo yatafanywa kwa kuzingatia amani na kwamba wakaazi watatembea hadi katika ofisi za Gavana Mung’aro ili kuwasilisha lalama zao.

“Tumechoka na hii shida ya uhaba wa maji iliyodumu kwa mwezi mmoja sasa na tutafanya maandamano hadi kwa ofisi za Gavana ili atueleza shida iko wapi, mbona wakaazi tunahangaika na uhaba wa maji”, alisema Rev. Katana.

Viongozi hao wa kidini pamoja na wakaazi wamelalamikia kutoangaziwa kwa maslahi yao licha ya kuwasilisha lalama kwa viongozi na wawakilishi wa maeneo yao, wakisema wakati umefika sasa kwa viongozi kuwajibika ama wananchi watatumia mamlaka yao ya kidemokrasia kuwatimua kazini.

Kwa upande wake Mwanasiasa Peter Ziro aliitaka serikali ya kaunti ya Kilifi kutatua changamoto hiyo mara moja ili kuwapungumzia mahangaiko wakaazi hao, akisema serikali ya kaunti iko na raslimali za kutosha za kuzikabili changamoto zinazowakumba wananchi mashinani.

“Tunashangaa na serikali hii ya Gavana Mung’aro, yani suala la maji ambalo ni uhai kwa wananchi waliyomchagua analichukulia kama jambo la mzaa, watu wanahitaji maji kwa matumizi ya kinyumbani na tukiendelea hivi basi tutateseka. Viongozi waliopewa jukumu la kushughulia maslahi ya wananchi ni lazima wawajibike kikamilifu”, alisema Ziro.

Akijubu lalama hizo zilizoibuliwa na wakaazi hao, Mkurugenzi wa Kampuni ya usambazaji maji ya Malindi, (MAWASCO) Felix Wanje alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo, akisema ilichangiwa na kukatwa kwa nguvu za umeme kutokana na deni la umeme ambalo bado halijalipwa.

“Changamoto kweli ipo na hiyo shida tunaishughulikia na wananchi watapata maji hivi karibuni. Tatizo hilo lilichangiwa na kukatwa kwa nguvu za umeme kutokana na deni ambalo bado tunadaiwa lakini tunalishughulikia suala hilo”, alieleza Wanje.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending