Connect with us

News

Kaunti ya Lamu yaandaa jukwaa la kuangamiza ukame

Published

on

Kaunti ya Lamu imeandaa Awamu ya Pili ya mkutano wa ngazi ya juu kwa ajili ya kuangazia mikakati ya kuangamiza ukame ambayo ni hatua muhimu kuelekea kuimarisha ustahimilivu wa muda mrefu na usimamizi wa kukabiliana na majanga katika kaunti nzima.

Mkutano huo ulioongozwa na Waziri wa Ardhi, maji na Nishati katika kaunti hiyo Tashrifa Abubakar, pamoja na wadau wa Mamlaka ya kitaifa ya kukabiliana na Ukame (NDMA) pia uliwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo mashirika ya serikali na washirika wa maendeleo.

Washiriki walielekezwa kuhusu vipengele muhimu vya mfumo wa awamu ya Pili ya kuangamiza ukame, unaolenga kuhamia kutoka hatua za dharura za kukabiliana na ukame kuelekea mifumo endelevu ya muda mrefu.

Washiriki wamethibitisha dhamira yao ya kuimarisha ushirikiano chini ya muundo wa jukwaa la uratibu katika ngazi ya kaunti- CSG, wakitambua kuwa ni jukwaa muhimu la kupanga kwa pamoja, kufanya maamuzi, na kutekeleza mipango.

Mkutano huo pia ulitumika kama jukwaa la kusherehekea utambuzi wa kimataifa wa hivi karibuni wa Kaunti ya Lamu kupitia Tuzo za Kimataifa za Water Transversality, ambapo Mpango wa Uondoaji Chumvi na Usimamizi wa Maji wa Kiunga ulitunukiwa kama Mradi Bora wa Athari kwa Jamii (2026).

Viongozi wa kaunti ya Lamu pamoja na Mamlaka ya kukabiliana na ukame na washkadau mbalimbali wanafanya kikao cha kuangazia mikakati ya kudhibiti ukame

Mradi wa Kiunga ni mfano bora wa ustahimilivu jumuishi unaoongozwa na jamii.

Awali ulianzishwa kufuatia uhaba mkubwa wa maji uliosababisha migogoro ya rasilimali, suala ambalo liliwasilishwa kwa jukwaa la uratibu katika ngazi ya kaunti kwa majadiliano.

Viongozi wamesisitiza kuwa mafanikio ya mradi wa Kiunga na utambuzi wake wa kimataifa yalitokana moja kwa moja na uratibu madhubuti chini ya mfumo wa Jukwaa hilo, ukiungwa mkono na Mamlaka ya Kitaifa ya kukabiliana na Ukame-NDMA.

Kaunti hiyo imethibitisha nafasi yake kama mfano bora wa jinsi mbinu jumuishi za sekta mbalimbali zinavyoweza kushughulikia kwa ufanisi changamoto za ukame, migogoro, na mabadiliko ya tabianchi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending