Sports
Serem ashinda shaba mashindano ya Riadha Duniani jijini Tokyo
Bingwa wa dunia kwa chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Edmund Serem ameishindia Kenya nishani ya shaba ya mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji katika mashindano ya Riadha Ulimwenguni leo Jumatatu jioni.
Serem amekamilisha mbio hizo kwa muda wa dakika 8 sekunde 34.56, ikiwa medali ya kwanza katika mbio za watu wazima.
Gordie Bimmish wa New Zealand ndiye bingwa mpya wa shindano hilo baada ya kutumia dakika 8 sekunde 33.88, akimlemea bingwa wa mwaka 2023 Soufiane El Bakkali wa Morocco, aliyeshinda fedha kwa dakika 8 sekunde 33.95.
Matokeo hayo yanaiacha Kenya ikiendeleza ukame wa dhahabu ya mbio hizo, tangu Consenslus Kipruto aliposhinda dhahabu mwaka 2019 mjini Doha, Qatar, akimrithi Ezekiel Kemboi aliyekuwa ameshinda dhahabu nne za mbio hizo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

