Connect with us

Sports

Seville Amshinda Lyles Lausanne, Wanyonyi Apata Pigo Katika Diamond League

Published

on

Mjamaica Oblique Seville alimshinda bingwa wa Olimpiki Noah Lyles katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Diamond League yaliyofanyika Lausanne jana usiku, ikiwa ni wiki tatu tu kabla ya mashindano ya dunia jijini Tokyo.

Mara nyingine tena, Lyles alichelewa kutoka kwenye vibao vya mwanzo, hali iliyompa Seville nafasi ya kuongoza mapema—aambayo Mjamaica huyo hakuwahi kuipoteza.

Seville alimaliza kwa muda wa kuvutia wa sekunde 9.87 chini ya mvua kubwa katika Stade Olympique de la Pontaise, huku Lyles akijaribu kujitahidi kurejea kwa mwendo wa kasi na kushika nafasi ya pili kwa sekunde 10.02. Hii ilikuwa marudio ya mashindano ya London Diamond League mwezi uliopita ambapo Seville mwenye umri wa miaka 24 pia alimshinda Mmarekani huyo.

“Nimemshinda bingwa wa Olimpiki mara mbili, London na hapa, na hilo linanipa imani kubwa kuelekea mashindano makuu. Imekuwa muda mrefu tangu Mjamaica kushinda mita 100 kwenye mashindano ya dunia, na bila shaka naamini mimi ndiye nitaifanya,” alisema Seville.

Lyles, kwa upande wake, alijilaumu akisema alihisi “mwitikio mbaya sana kwenye bastola ya kuanzia. Hilo ndilo kosa pekee.”

“Kiufundi nilihisi niko vizuri, mazoezi ya kujiandaa yalikuwa mazuri, lakini ukichelewa kuanza kwenye kiwango hiki, basi mbio huwa zimeisha,” aliongeza.

“Kimwili nahisi niko vizuri, na nina imani kila mbio zitanipa mwendelezo bora zaidi. Lengo ni kuboresha maelezo madogo hasa mwendo wa mwanzo na kasi yangu ya kwanza kuelekea Tokyo na mashindano ya dunia.”

  • Hoey aongoza –

Bingwa wa Olimpiki kutoka Kenya kwenye mita 800 Emmanuel Wanyonyi pia alipata pigo baada ya Mmarekani Josh Hoey kushinda mbio hizo.

Hoey, bingwa wa dunia wa ndani ya ukumbi (indoor), alijihakikishia ushindi katika mita za mwisho na kumaliza kwa muda wa dakika 1:42.82.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending