Sports
Seville Amshinda Lyles Lausanne, Wanyonyi Apata Pigo Katika Diamond League
Mjamaica Oblique Seville alimshinda bingwa wa Olimpiki Noah Lyles katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Diamond League yaliyofanyika Lausanne jana usiku, ikiwa ni wiki tatu tu kabla ya mashindano ya dunia jijini Tokyo.
Mara nyingine tena, Lyles alichelewa kutoka kwenye vibao vya mwanzo, hali iliyompa Seville nafasi ya kuongoza mapema—aambayo Mjamaica huyo hakuwahi kuipoteza.
Seville alimaliza kwa muda wa kuvutia wa sekunde 9.87 chini ya mvua kubwa katika Stade Olympique de la Pontaise, huku Lyles akijaribu kujitahidi kurejea kwa mwendo wa kasi na kushika nafasi ya pili kwa sekunde 10.02. Hii ilikuwa marudio ya mashindano ya London Diamond League mwezi uliopita ambapo Seville mwenye umri wa miaka 24 pia alimshinda Mmarekani huyo.
“Nimemshinda bingwa wa Olimpiki mara mbili, London na hapa, na hilo linanipa imani kubwa kuelekea mashindano makuu. Imekuwa muda mrefu tangu Mjamaica kushinda mita 100 kwenye mashindano ya dunia, na bila shaka naamini mimi ndiye nitaifanya,” alisema Seville.
Lyles, kwa upande wake, alijilaumu akisema alihisi “mwitikio mbaya sana kwenye bastola ya kuanzia. Hilo ndilo kosa pekee.”
“Kiufundi nilihisi niko vizuri, mazoezi ya kujiandaa yalikuwa mazuri, lakini ukichelewa kuanza kwenye kiwango hiki, basi mbio huwa zimeisha,” aliongeza.
“Kimwili nahisi niko vizuri, na nina imani kila mbio zitanipa mwendelezo bora zaidi. Lengo ni kuboresha maelezo madogo hasa mwendo wa mwanzo na kasi yangu ya kwanza kuelekea Tokyo na mashindano ya dunia.”
-
Hoey aongoza –
Bingwa wa Olimpiki kutoka Kenya kwenye mita 800 Emmanuel Wanyonyi pia alipata pigo baada ya Mmarekani Josh Hoey kushinda mbio hizo.
Hoey, bingwa wa dunia wa ndani ya ukumbi (indoor), alijihakikishia ushindi katika mita za mwisho na kumaliza kwa muda wa dakika 1:42.82.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

