Sports
Shabiki Apigwa Marufuku Viwanja Vyote Uingereza kwa Kumtusi Kibaguzi Antoine Semenyo
Mwanaume mmoja aliyekamatwa kwa tuhuma za kumtolea matusi ya kibaguzi mshambuliaji wa Bournemouth, Antoine Semenyo, wakati wa mechi ya ufunguzi ya Ligi Kuu ya Uingereza kwenye uwanja wa Anfield, amepigwa marufuku kuingia kwenye viwanja vyote vya mpira wa miguu nchini Uingereza.
Mchezo wa Bournemouth dhidi ya Liverpool siku ya Ijumaa ulisitishwa kwa muda dakika ya 29 baada ya Semenyo kumjulisha mwamuzi kuhusu tukio hilo.
Kwa mujibu wa Polisi wa Merseyside, mwanaume mwenye umri wa miaka 47 kutoka Liverpool alikamatwa Jumamosi kwa tuhuma za kosa la utovu wa nidhamu lenye misingi ya kibaguzi, na kwa sasa ameachiliwa kwa dhamana yenye masharti.
Masharti hayo ni pamoja na marufuku ya kuhudhuria mechi yoyote ya mpira wa miguu iliyoidhinishwa nchini Uingereza na kutoruhusiwa kwenda umbali wa ndani ya maili moja kutoka uwanja wowote ulioteuliwa wa mpira wa miguu.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

