Sports
Sinner Bingwa Tennis Msururu Wa Wimbledon
Mchezaji wa Tenisi anayeorodheshwa wa kwanza Ulimwenguni Jennik Sinner raia wa Italia amesema kwamba lengo lake ni kutawala dunia sasa baada ya kumpiku mwenzake Carlos Alcaraz na ksuhinda fainali ya taji la Wimbledon likiwa ni taji lake la kwanza.
Sinner alimpiku Alcaraz raia wa Uhispania kwa seti za 4-6, 6-4, 6-4, 6-4 na kuvunjilia mbali rekodi ya mhispania huyo ya kushinda taji hilo mara tatu mfululizo.
Mchezaji huyo amesema kwamba analenga kujiboresha hata zaidi akiwaonya wapinzani angali kutoa makali yake yote.
“Niko na umri wa miaka 23 na kwa sasa ningali kuwa katika ubora wangu narudi kujipanga zaidi kwa ajili ya misururu mingine ila niko na imani ya kufanya kweli katika misuru ya Tenisi.”
Mchezaji huyo amfika katika fainali nne na kushinda tatu za Grandslam na amesema hataki kutoka hapo juu kuwa mchezaji bora.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

