Sports
Super Eagles Yaaga CHAN Baada ya Kuchapwa 4–0 na Sudan
Timu ya taifa ya Nigeria, maarufu kama Super Eagles, imeaga mashindano ya CHAN baada ya kuchapwa mabao 4–0 na Sudan katika mechi ya pili ya Kundi D iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Amaan Sports Complex, Zanzibar.
Sudan walichukua uongozi mapema dakika ya 21 ya kipindi cha kwanza kupitia goli la kujifunga kutoka kwa beki Leonard Ngenge, kabla ya kuongeza bao la pili dakika ya 44 kupitia nahodha Walieldin Khedr aliyefunga kwa mkwaju wa penalti.
The Nile Crocodiles walirejea kipindi cha pili wakiwa moto wa radi, ambapo mshambulizi Abdel Raouf alifunga bao la tatu dakika ya 55 na kuongeza la nne dakika ya 62, kukamilisha kipigo kizito kwa Nigeria.
Huu ulikuwa mchuano ulioshuhudia idadi kubwa zaidi ya mabao katika mashindano hayo hadi sasa. Super Eagles walihitaji matokeo chanya ili kuendeleza matumaini ya kusonga mbele, baada ya kupoteza mechi ya ufunguzi kwa bao 1–0 dhidi ya Senegal.
Katika mchezo mwingine wa Kundi D uliochezwa jana, Senegal walitoka sare ya 1–1 na Congo Brazzaville.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

