Sports
Thomas Frank Kocha Mpya Spurs!
Kilabu ya Tottenham Hotspurs kumtangaza kocha wa sasa wa Brenford Thomas Frank kuwa kocha mpya wa kilabu hiyo kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu wiki jana kutokana na msururu wa matokeo duni.
Kulingana na mkali wa taarifa Uhamisho barani Ulaya Fabrizio Romano ni kwamba makubaliano ya pande zote mbili zimafikiwa huku Spurs wakiwa tayari kulipia ada ya pauni milioni 10 ikiwa ni kifungu kilichomo kwenye mkataba wa kocha huyo kabila kukamilisha usajili huo.
Duru za kuaminika zaarifu kwamba mwalimu huyo amekubaliana na kilabu hiyo kwa matakwa ya binafsi na yuko tayari kuanza upya na kilabu hiyo ya London Kaskazini msimu ujao.
Raia huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 51 aliongoza Brenford kumaliza kumi bora msimu uliopita na alama 56.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

