Connect with us

Sports

Torres aibeba Barcelona kwa mabao mawili, Atletico yakwama kwa sare na Mallorca

Published

on

Mshambulizi Ferran Torres alifunga mabao mawili kwa mabingwa Barcelona walipoichapa Getafe 3-0 Jumapili na kusalia nyuma ya Real Madrid kileleni mwa La Liga.

Dani Olmo pia alifunga bao kwa upande wa Wacatalunya, ambao sasa wako pointi mbili nyuma ya vinara Madrid baada ya kikosi cha Xabi Alonso kuishinda Espanyol Jumamosi na kudumisha rekodi yao ya ushindi wa asilimia 100.

Mwanzo wa msimu wenye kusuasua kwa Atletico Madrid uliendelea baada ya kutoka sare ya 1-1 na Mallorca, huku mshambuliaji wao Julian Alvarez akikosa penalti.

Wakicheza tena katika uwanja wa Johan Cruyff wenye uwezo wa watazamaji 6,000 ulio karibu na kituo chao cha mazoezi, wakati klabu ikisubiri leseni za kufunguliwa kwa uwanja wao uliokarabatiwa wa Camp Nou, Barcelona walitawala mchezo dhidi ya Getafe waliokuwa wakicheza bila ubunifu.

Licha ya kufunga mabao mawili dhidi ya Newcastle kwenye Ligi ya Mabingwa, kocha Mjerumani Hansi Flick alimwacha Marcus Rashford benchi, huku vyombo vya habari vya Uhispania vikiripoti kwamba ilikuwa kwa sababu mshambuliaji huyo wa England alichelewa kwenye kikao cha asubuhi.

Flick tayari amewahi kuwaadhibu wachezaji wengine kwa kosa kama hilo hapo awali, akiwemo beki Jules Kounde.

“(Mzunguko wa wachezaji) ni jambo la kawaida kwa sababu kila baada ya siku tatu au nne tunakuwa na mechi, tunahitaji miguu mipya uwanjani,” Flick alisema alipoulizwa kwa nini Rashford hakuanza.

Mbadala wa Rashford, aliyemrithi kijana nyota aliyeumia Lamine Yamal, alikuwa Torres — na alitumia nafasi yake ipasavyo.
“Tunazo mechi nyingi kwa hiyo ni jambo jema kuwa na kila mchezaji akicheza kwa kiwango hiki,” Flick aliongeza.

Mchezaji huyo wa Uhispania alifungua ukurasa wa mabao kwa shuti kali baada ya mpira uliopigiwa kisigino na Olmo ndani ya boksi.

Bao la pili la Torres lilikuwa zuri zaidi, akielekeza mpira kwa ustadi pembe ya kushoto chini ya lango baada ya kupigiwa pasi safi na Raphinha.

Mbele, alikaribia kutia kapuni hat-trick ya kipindi cha kwanza alipogonga mwamba kwa shuti kali.

Wachezaji kadhaa wa Barca walionekana kukasirika kabla ya mapumziko baada ya Getafe kufanya makosa mengi ya rafu kali, huku Kounde akiwa mhanga zaidi.

Flick alimpumzisha Raphinha na kumwingiza Rashford kipindi cha pili, huenda kumlinda Mbrazil huyo asipate kadi nyekundu.

“Mara nyingi hawajaribu chochote isipokuwa makosa ya rafu nyingi, kwa maoni yangu, lakini tuliweza kushughulikia vizuri,” Torres aliambia DAZN.

“Niliwaambia wachezaji: lazima tuzingatie mchezo wetu, si wao,” alisema Flick.

Rashford alisaidia bao la tatu la Barcelona, akipenya upande wa kulia na kumpasia Olmo pasi safi ya kufunga, kisha yeye mwenyewe akijaribu mara mbili lakini akazuiwa na kipa wa Getafe, David Soria.

Habari mbaya pekee kwa Barca ilikuwa mchezaji wa akiba Fermin Lopez kuonekana kupata jeraha dakika za majeruhi.

Atletico Wakata Tamaa
Mapema, Atletico walikwama kwa sare dhidi ya Mallorca licha ya kuwazidi wenyeji.

Kikosi cha Diego Simeone kilipunguzwa hadi wachezaji 10 baada ya Alexander Sorloth kuonyeshwa kadi nyekundu, lakini walitangulia kwa bao la Conor Gallagher kabla ya Vedat Muriqi kusawazisha dakika ya 85.

Kilabu hiyo ikisalia nafasi ya 14 mpaka sasa ligi ya LALIGA na alama 5

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending