Sports
Uganda Yaponea Chupu Kuingia Robo Fainali Mashindano ya CHAN
Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) yaliendelea kwa michezo yenye ushindani mkubwa ambapo Uganda na Afrika Kusini walitoka sare ya kufungana mabao 3-3 katika mchezo uliokuwa wa kusisimua mno.
Mchezo huo uliochezwa jana ulivutia mashabiki kutokana na kasi na mashambulizi ya pande zote mbili, huku kila timu ikionyesha dhamira ya kusaka ushindi. Uganda walitangulia mara mbili, lakini Afrika Kusini waliendelea kusawazisha hadi kufikia matokeo ya 3-3 kufikia mwisho wa dakika 90.
Katika mchezo mwingine, wenyeji Algeria walishindwa kutamba mbele ya Niger baada ya kutoka sare tasa ya 0-0. Licha ya kupewa nafasi kubwa kutokana na kuwa nyumbani, Algeria walikosa kutumia fursa walizopata, huku Niger wakicheza kwa nidhamu ya hali ya juu kuhakikisha wanabeba alama moja muhimu.
Kwa matokeo haya, Uganda Cranes sasa wamefuzu kwa robo fainali baada ya kumaliza kileleni na alama saba,Algeria imemaliza ya pili na alama sita huku Afrika kusini wakimaliza ya tatu na alama sita huku Niger na Guinea pia wakiaga mashindano hayo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

