Sports
Vilabu Vinavyoshriki Mashindano Ya CAF Kuvuna Maradufu
Ni Afueni kwa vilabu vya Kenya Police na Nairobi United vinavyowakilisha nchi kwenye mashindano ya kilabu bingwa barani (CAF Champions Ligi) na taji la mashirikisho (CAF Confederation) mtawalia.
Hii ni baada ya shirikisho la soka Barani Afrika CAF kutangaza ongezeko la asilimia 100 ya kipato ambacho vilabu vilikua vinavuna misimu ya nyuma.
vilabu vyote 130 vinatarajiwa kunufaika na ongezeko hilo ambapo vilabu ambavyo vilipokea dolla 50,000 sawa na shilingi milioni 6.4 na ya Kenya sasa vitapokea Dolla Milioni 100,000 sawa na Milioni 12.4 ya Kenya.
Hatua hii mpya iliotangazwa na Rais wa CAF Patrice Motsepe itasaidia pakubwa vilabu katika usafiri na maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo kwa jumla.
Kenya inawakilishwa na kenya Police Ligi ya Mabingwa Barani huku Nairobi United wakilisha katika taji la mashirikisho Barani Afrika.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

