Sports
Vilabu Vya KCB Na GSU Mabingwa Taji La Kenya Cup
Kilabu ya wanabenki KCB ya wanawake ndiyo mabingwa wa Voliboli taji mpya la Kenya Cup fainali iliopigwa ugani Kasarani Indoor Arena wikendi hii.
Hii ni baada ya vipusa hao wa kocha Japheth Munala kuwashinda Kenya Pipeline kwa seti 3-0 za 25-16,25-19,25-22 katika fainali kali ilipigwa katika uga huo
Kwa mujibu wa kocha huyo ni kwamba haikua mechi rahisi kwao na mabingwa wa taji la ligi ya Voliboli nchini Kenya Pipeline ila walikua wamejipanga vizuri kwa mechi hiyo kuliko mechi yoyote ile.
“Tunaheshimu sana wapinzani wetu,ila niliambiwa wachezaji wangu wamejitoe zaidi kwani nilijua si mechi rahisi dhidi ya Pipeline kwani ni timu nzuri mno.”
Katika upande wa wanaume kilabu ya GSU ilinyuka WanaKDF seti 3-0 za 25-22,26-24,25-17 na kuibukia mabingwa wa kombe hilo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

