Connect with us

Business

Wadau wa Sekta ya Uchumi wa Baharini Waisihi Serikali Kuongeza Uwekezaji Pwani

Published

on

Wadau katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa katika eneo la Pwani wameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kusaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa wadau hao, serikali haijatoa kipaumbele cha kutosha kwa sekta hiyo, licha ya kuwepo kwa raslimali nyingi za bahari ambazo bado hazijatumika ipasavyo. Wamesisitiza kuwa uwekezaji wa kimkakati unaweza kufungua fursa nyingi kwa vijana, na hivyo kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira katika ukanda wa Pwani.

Viongozi hao pia wameitaka serikali, kupitia wizara husika, kuweka mikakati ya wazi na ya utekelezaji ili kuhakikisha kwamba wananchi—hasa vijana—wanapata nafasi ya kunufaika na uchumi wa buluu.

Wakati huo huo, wamewahimiza vijana wa Pwani kujipanga na kujitolea kwa dhati, ili wawe tayari kutumia fursa zinazojitokeza katika sekta ya uchumi wa bahari kwa manufaa yao binafsi na ya jamii kwa ujumla.

Sekta ya uchumi wa buluu inazidi kutambuliwa kama eneo muhimu la ukuaji wa uchumi, hasa kwa maeneo ya pwani yanayozungukwa na bahari, mito na maziwa makuu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko

Published

on

By

Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.

Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.

Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.

Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.

Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.

“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending