Connect with us

Business

Wafanyabiashara Wakosoa KRA Kuhusu Ushuru wa Juu na Huduma Duni

Published

on

Baadhi ya wafanyibiashara mjini Malindi kaunti ya Kilifi wanalalamikia kupanda kwa gharama ya maisha sawa na ushuru wa biashara wakati mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini, KRA ikitangaza ongezeko la ukusanyaji wa ushuru kwa asilimia 6.8 katika mwaka wa kifedha 2024/2025.

Wakiongozwa na Kenza Ondiek wafanyibiashara hao wanasema kuwa ongezeko la ushuru nchini limeathiri pakubwa ustawi wa biashara huku uboreshaji wa miundomsingi ukiwa katika viwango vya chini.

Ondiek ameiomba serikali kuhakikisha kuwa inaboresha maisha ya wananchi kupitia mapato ya ushuru hasa baada ya mamlaka ya KRA kukusanya jumla ya shilingi trilioni 2.61 katika mwaka wa kifedha 2024/2025 ikilinganishwa na trilioni 2.40 za mwaka kifedha 2023/2024.

Ondiek aidha ameiomba serikali kuwajibikia kikamilifu matumizi bora ya fedha za ushuru zinazokusanywa nchini ili kubadilisha maisha ya wananchi badala ya kuangazia njia za kuongeza kiwango cha makato ya ushuru pekee kwa wananchi.

Haya yanajiri huku mamlaka ya KRA pia ikifichua kupitisha makadirio yake ya ukusanyaji wa ushuru kutoka kwa shilingi trilioni 2.56 hadi shilingi trilioni 2.61 kwa mwaka wa kifedha 2024/2025.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending