Sports
Wakenya Kuzindua Uhasama Mbio Za Oregon Prefontaine Classic
Wanariadha nguli wa Kenya watatumia mbio za makala ya Oregon Prefontaine Classic kama mbio za majaribio kabila ya mbio za Dunia mjini Tokyo Japan badaye mwakani.
Bingwa wa Olimpiki mbio za mitaa 5000 na 10,000 Batrice Chebet anatarajiwa kuongoza wenzake katika mbio hizo wikendi hii ambapo chama cha riadha AK inatarajiwa kukiteuwa kikosi chake cha dunia.
Wanariadha wengine ambao wanarajiwa kutimka mbio hizo mjini Oregon Marekani ni pamoja na ;bingwa wa mbio za kilomita 10 Agnes Ngetich,bingwa wa zamani mbio za mitaa 10000 Caroline Nyaga,wengine ni pamoja na: Margaret Akidor, Maurine Jepkoech, Janeth Chepngetich, Sarah Wanjiru, Caroline Kariba, na Hellen Ekalale.
Sheria za chama Raidha nchini AK zinaarifu kwamba washindi watakaomaliza nafasi za kwanza na ya pili wanafuzu moja kwa moja katika mashindano ya Dunia.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

