Sports
Wanaridha Beatrice Chebet,Faith kipyegon,Emmanuel Wanyonyi na Lilian Odira warejea kutoka Tokyo
Mabingwa wa Dunia Faith Kipyegon, Beatrice Chebet, Lillian Odira na Emmanuel Wanyonyi wamerejea nyumbani leo kutoka Tokyo, Japan, walikoshiriki mashindano ya Riadha Duniani.
Familia, ndugu, jamaa na rafiki pamoja na maafisa wa serikali walijitokeza kuwapokea mashujaa hao katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta.
Wakizungumza, Kipyegon na Chebet walisema wanaazimia kusalia katika mbio za uwanjani kabla ya kuhamia barabarani.
“Nafurahia sana kushinda dhahabu ya nne katika mbi za mita 1,500 na pia kuwamotisha akina dada wengine kwa sababu mimi ni kama mama yao. Beatrice amekuwa akitazama nikikimbia, na saa hii tunakimbia naye,” akasema Kipyegon.
Aidha Chebet amesema aangazia kushinda medali zaidi katika mita 5,000 na 10,000, huku akisema ushirikiano wa kikosi cha Kenya ulichangia matokeo.
Odira amesema anajipanga sasa kushiriki mashindano ya Ultimate mwaka ujao baada ya kutwaa ubingwa wa Dunia.
Kenya ilimaliza ya pili katika msimamo wa nishani kwa dhahabu 7, fedha 2 na shaba 2.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

