Connect with us

Sports

Wanyonyi, Cherotich na Chepchirchir Washinda Fainali Diamond League Zurich, Kenya Yaandika Historia

Published

on

Bingwa mtetezi wa Olimpiki katika mbio za mita 800, Emmanuel Wanyonyi, aliibuka mshindi wa taji la Diamond League baada ya kumshinda  Max Burgin wa Uingereza katika fainali ya mbio hizo jijini Zurich, jana usiku.

Wanyonyi, ambaye anasubiri Kipute cha Dunia mjini Tokyo Japan ndani ya wiki mbili zijazo, alilazimika kutumia kasi ya mwisho ili kuzuia shambulizi la kasi la Mwingereza huyo katika hatua ya kumalizia. Akishinda kwa muda bora wa 1:42.37, huku Burgin akimaliza kwa muda wa 1:42.42.

Bingwa mtetezi wa Diamond League, Marco Arop wa Canada, alimaliza wa tatu kwa muda wa 1:42.57.

Ushindi wa Wanyonyi ukiashiria usiku wa kihistoria kwa Kenya, ambapo timu hiyo ilitwaa jumla ya medali tatu za Diamond League na medali ya fedha.

Mkenya mwingine Faith Cherotich, bingwa wa medali ya shaba Olimpiki, alidhibitisha umahiri wake kama malkia wa mbio za 3000m kuruka viunzi na maji, akitetea taji lake kwa muda wa 8:57.24.

Akiwa amefunzwa na Bernard Rono katika kituo cha mazoezi cha Kalyet, Kericho, bingwa wa zamani wa dunia kwa vijana aliwashinda kwa ufasaha Norah Jeruto mwenye asili ya Kenya lakini anayewakilisha Kazakhstan (9:10.87), na Marwa Bouzayani wa Tunisia (9:12.03).

Kocha Rono alimpongeza akisema: “Tulikuwa na malengo, na taji la Diamond League lilikuwa shabaha kuu. Sasa tuna siku chache kurekebisha maandalizi yetu kabla ya mashindano ya Dunia.”

Mwanariadha Nelly Chepchirchir, anayefundishwa na gwiji wa mita 800 Janeth Jepkosgei, aling’aa katika mbio za mita 1500 wanawake, akipiga kasi ya ajabu katika raundi ya mwisho na kutwaa taji lake la kwanza la Diamond League.

Alikimbia kwa muda wa 3:56.99, baada ya kumpita Jess Hull wa Australia, aliyekuwa anaongoza mbio kwa muda mrefu lakini akalemewa mwishoni.

Vijana pia walionesha makali, ambapo Edmund Serem mwenye umri wa miaka 17, mdogo wake Amos Serem (bingwa wa Diamond League 2024), alionesha kina cha vipaji vya Kenya katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji.

Serem mdogo alikimbia 8:09.96, akinyakua fedha, nyuma kidogo ya Frederik Ruppert wa Ujerumani (8:09.02). Tayari akiwa sehemu ya kikosi cha Kenya kitakachoshiriki mashindano ya Dunia mjini Tokyo, kijana huyo alionesha yuko tayari kuwakabili wakali wa dunia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending