Connect with us

Sports

Harambee Stars Wapiga Ushelisheli Kasarani, Olunga Asawazisha Rekodi ya Oliech

Published

on

Timu ya soka Harambee Stars hatimaye wamehitimisha kusubiri ushindi wa nyumbani kwenye kufuzu Kombe la Dunia 2026 baada ya kushinda kwa kishindo cha mabao 5-0 dhidi ya UShelisheli katika uwanja uliojaa mashabiki wa Kasarani Jumanne alasiri.

Kocha mkuu Benni McCarthy alifanya mabadiliko sita kutoka kwa kikosi kilichopoteza 3-1 dhidi ya Gambia wiki iliyopita. Kipa Brian Bwire alimchukua nafasi Byrne Omondi langoni, huku Ronney Onyango akibaki beki wa kulia.

Kwa kuwa Aboud Omar alikuwa amesimamishwa, Manzur Okwaro alicheza katika nafasi yake ya asili kama beki wa kushoto mabadiliko yaliyokaribishwa baada ya kuonesha uwezo mkubwa katika michuano ya CHAN 2024 kama kiungo mkabaji. Kwenye moyo wa safu ya ulinzi, Sylvester “Sili” Owino na Collins Shichenje waliendeleza ushirikiano wao, wakilindwa na Alpha Chris Onyango, aliyemchukua nafasi Richard Odada. Aliungana na Duke Abuya katikati ya uwanja, huku Ryan-Wesley Ogam akichukua nafasi ya Timothy Ouma Noor, akicheza kama namba tisa ya uongo.

Job Ochieng’, aliyeng’aa alipoingia kama mchezaji wa akiba dhidi ya Gambia, alianza kwenye wingi wa kushoto mbele ya Emmanuel Osoro, huku Wilson Lenkupae anayekipiga Australia akicheza wingi wa kulia. Nahodha Michael Olunga aliongoza safu ya mashambulizi.

Mashabiki hawakungojea kwa muda mrefu. Dakika ya 7, nyota wa moto Ogam alivunja kimya kwa kumalizia kwa ustadi.

Kenya walimiliki mpira na kuongeza bao la pili dakika ya 35 kupitia Collins Shichenje aliyemalizia pasi ya Abuya. Dakika tatu baadaye, Ogam alifunga tena — bao lake la nne katika mechi sita pekee — na kufanya matokeo kuwa 3-0. Kabla ya mapumziko, Olunga alifunga kwa mkwaju wa penalti baada ya Ogam kuangushwa ndani ya kisanduku, na kuwapa Stars uongozi wa 4-0 kipindi cha kwanza.

Bao hilo lilimfanya Olunga kufikia rekodi ya Dennis Oliech ya mabao 34, na kumfanya awe mfungaji wa pili bora wa muda wote wa Kenya kwa pamoja.

Kipindi cha pili, McCarthy aliwatoa Ochieng’, Lenkupae na Abuya na kuwaingiza Ben-Stanley Omondi, Boniface Muchiri na Marvin Nabwire. Mabadiliko hayo yalizaa matunda dakika ya 68, Olunga aliporuka juu na kufunga kwa kichwa kutoka krosi safi ya Onyango, na kuhitimisha ushindi wa 5-0.

Licha ya Kenya kutokuwa na nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 nchini Marekani, Kanada na Mexico, ushindi huu uliwaweka katika nafasi ya nne Kundi F wakiwa na pointi 9 — moja nyuma ya Burundi na mbili juu ya Gambia, waliotarajiwa kukutana usiku huo. Stars sasa wanageuza macho yao kwenye mechi za mwisho za kufuzu mwezi Oktoba, ambapo watakutana na Burundi (Okt 6) na vinara wa kundi Ivory Coast (Okt 13).

Ivory Coast kwa sasa wanaongoza kundi wakiwa na pointi 19, wakiwa pointi moja mbele ya Gabon walioko nafasi ya pili.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending