Sports
Bandari Yampiga kalamu kocha wake Ken Odhiambo baada ya mechi 2 Tu
Kilabu ya Bandari ya Pwani imetangaza kumpiga kalamu kocha wake mkuu Ken Odhiambo baada ya mechi mbili pekee usukani msimu huu.
Haya yanajiri saa chache tu baada ya kilabu hiyo kupoteza goli 1-0 dhidi ya Shabana siku ya Jumapili ugani Mbaraki kaunti ya Mombasa.
Mwalimu huyo aliongoza The Dockers kumaliza nafasi ya nane msimu jana na alama 44 matokeo ambayo hayakupokelewa vema na uongozi wa kilabu hiyo.
Hata hivyo licha ya kupewa nafasi kubadilisha mambo baada ya kupata wachezaji wapya matokeo yanaonekana vinginevyo kilabu hiyo ikiwa na alama moja pekee kutokana na mechi 2 za FKF PL.
Naibu kocha John Baraza amepewa usukani wa kuongoza kilabu hiyo huku harakati ya kusaka kocha mpya kilabuni humo ikianza rasmi wadadisi wakisema kilabu hiyo sasa inasaka kocha wa kigeni.
Mechi ijayo ya kilabu hiyo ni dhidi ya Muranga Seal.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

