Connect with us

Business

Bei za Vitunguu kupanda zaidi msimu huu

Published

on

Bei za baadhi ya bidhaa humu nchini zinatarajiwa kupanda hata zaidi msimu huu ikilinganishwa na hapo awali.

Wafanyibiashara wanaoagiza bidhaa kutoka nchi jirani Tanzania mjini Kilifi walisema bidhaa kama vile kitunguu zinatarajwa kupanda bei kutokana na maandamano ambayo yalishuhudiwa hivi karibuni.

Kulingana na wafanyibiashara hao hali ilivyo kwa sasa katika taifa la Tanzania hawawezi kuingia katika taifa hilo kununua na hata kuangiza bidhaa kutoka nchi hiyo.

Kwa sasa kilo ya kitunguu inauzwa kwa shilingi 100 katika soko la Kwa Charo wa mae mjini Kilifi sawa na soko la mazeras kaunti ya Kilifi bei ambayo inatarajiwa kupanda.

Hata hivyo walitolea wito wakulima wa humu nchini kuendeleza kilimo cha Kitunguu kwa wingi ili kukoma kutengemea Kitunguu kutoka nchi jirani ya Tanzania.

“Biashara inatarajiwa kuwa ngumu kwani kupata bidhaa ambazo tunatarajia kutoa Tanzania itakuwa ngumu kwani wengi wanaogopa kuingia katika nchini hiyo.

‘”Wakulima wa humu nchini lazima waongeze kiwango cha kitunguu wanachopanda ili kusaidia hali hii”.

Taarifa ya Pauline Ngome

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko

Published

on

By

Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.

Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.

Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.

Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.

Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.

“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending