Connect with us

Sports

Calafiori Aipa Arsenal Ushindi Dhidi ya Man United; Chelsea Wakwama Kwa Sare Tasa na Palace

Published

on

Safari ya Arsenal kutafuta ubingwa wa Ligi Kuu ya EPL ilianza kwa ushindi muhimu baada ya bao la Riccardo Calafiori kuipa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Manchester United, Jumapili. Wakati huo huo, mabingwa wa dunia Chelsea walinusurika kwa sare tasa ya 0-0 dhidi ya Crystal Palace ugani Darajani.

Baada ya kumaliza katika nafasi ya pili kwa misimu mitatu mfululizo, presha iko kwa kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, kuhakikisha analeta taji la kwanza la ligi kwa klabu hiyo tangu msimu wa 2003/04.

Ingawa hawakuwa wa kuvutia sana uwanjani Old Trafford, Arsenal walijinyakulia alama tatu muhimu kufuatia kosa kubwa la kipa wa muda wa United, Altay Bayindir. Mlinda lango huyo wa kimataifa wa Uturuki alishindwa kudaka kona ya Declan Rice dakika ya 13 na kumwachia Calafiori nafasi rahisi ya kufunga kwa kichwa.

“Matokeo makubwa,” alisema Arteta. “Mchezo wa kwanza wa msimu, na ukiwa Old Trafford ambapo unahisi wanajaribu kujenga kitu.”

United waliwapa nafasi ya kwanza washambuliaji wapya waliogharimu pauni milioni 200 — Matheus Cunha, Bryan Mbeumo na Benjamin Sesko — lakini walishindwa kupenya ukuta wa ulinzi wa Arsenal ambao ndio bora zaidi kwa misimu miwili iliyopita.

Patrick Dorgu alipiga shuti kali lililogonga mwamba na kukaribia kuisawazishia United, huku kipa wa Arsenal, David Raya, pia akifanya kazi kubwa kuzuia juhudi za Cunha na Mbeumo.

“Tumethibitisha leo kuwa tunaweza kushinda mechi yoyote ya EPL dhidi ya timu kubwa kama Arsenal,” alisema kocha wa United, Ruben Amorim. “Tulistahili matokeo tofauti, lakini tunapaswa kuangalia mbele kwa mchezo unaofuata.”

Kizungumkuti cha Chelsea;

Chelsea walionekana bado kuchoka baada ya mafanikio ya Klabu Bingwa Dunia huku wakikwamishwa na washindi wa Kombe la FA, Crystal Palace. Bao la mapema la Palace kupitia mpira wa adhabu wa Eberechi Eze lilikataliwa na VAR kwa madai kuwa Marc Guehi aliizuia ngome ya Chelsea.

Licha ya uvumi kwamba wanatazamiwa kujiunga na Liverpool na Tottenham mtawalia, nyota wa Palace, Guehi na Eze, bado walianza mchezo huo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy

Published

on

Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.

Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.

Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.

“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.

Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.

Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.

Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.

Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

Continue Reading

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Trending