Connect with us

Sports

Cape Verde Yashangaza Cameroon, Yakaribia Kufaulu kufuzu Kombe la Dunia kwa Mara ya Kwanza

Published

on

Visiwa vya Cape Verde, taifa dogo la kisiwa Afrika Magharibi lenye idadi ya watu wasiozidi 550,000, iliishinda Cameroon 1-0 siku ya Jumanne na kuimarisha matumaini ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.

Timu hiyo kwa jina la utani Blue Sharks wanahitaji alama tatu mwezi Oktoba kutoka mechi dhidi ya Libya na nyumbani dhidi ya Eswatini ili kushinda Kundi D, ambalo lilitarajiwa kudhibitiwa na Cameroon waliowahi kufuzu Kombe la Dunia mara nane.

Mshambuliaji anayekipiga Italia, Dailon Livramento, mwenye umri wa miaka 24 aliyezaliwa Rotterdam kwa wazazi wa Cape Verde, ndiye aliyeibuka shujaa mjini Praia baada ya kufunga bao la ushindi dakika ya 54. Hilo lilikuwa bao lake la tatu katika kufuzu Kombe la Dunia 2026, baada ya mabao mawili yaliyoiwezesha Cape Verde kupata ushindi wa kushtua dhidi ya Angola Machi iliyopita.
Ushindi dhidi ya Cameroon ulikuwa wa furaha zaidi baada ya Indomitable Lions kushinda 4-1 walipokutana Yaoundé mwaka jana.

Cape Verde wana pointi 19, nne mbele ya Cameroon, ambao watakabiliana na Mauritius ugenini na kisha kuwakaribisha Angola katika raundi mbili za mwisho za mchujo wa kufuzu ulioanza mwaka 2023.

Cameroon, ambao wamefuzu mara nane kwenye michuano ya dunia (rekodi ya Afrika), walipata pigo mara mbili kwani sasa wameshuka hadi nafasi ya tano miongoni mwa timu zilizoshika nafasi ya pili. Ni timu nne pekee zilizoshika nafasi ya pili zenye rekodi bora ndizo zitakazofuzu kwa mchuano mdogo, ambapo mshindi ataenda kucheza mchujo wa mabara mwezi Machi kwa nafasi mbili za Kombe la Dunia.

Kwa Cape Verde, kuwa ukingoni mwa kufuzu kwa mara ya kwanza Kombe la Dunia ni mabadiliko makubwa, baada ya kushika mkia kwenye kundi la kufuzu AFCON 2025 kwa kushinda mechi moja pekee kati ya sita.

Kocha wa timu hiyo Pedro Leitao Brito, anayejulikana kwa jina maarufu Bubista (miaka 55), amekuwa akiinoa timu ya taifa tangu 2020. Nahodha ni mshambuliaji anayecheza Uturuki Ryan Mendes, mwenye miaka 35.

Cape Verde wanashikilia nafasi ya 73 duniani, nafasi 22 nyuma ya Cameroon waliowahi kuwa mabingwa wa Afrika mara tano. Mafanikio yao bora ya kimataifa ni kufika robo-fainali ya AFCON mwaka jana.

Senegal walipindua meza 
Senegal walipindua matokeo kutoka nyuma kwa mabao mawili na kushinda DR Congo 3-2 mjini Kinshasa, na kuongoza Kundi B kwa tofauti ya pointi mbili.

Cedric Bakambu na sajili mpya wa Newcastle United Yoane Wissa waliwafungia wenyeji kabla ya kurejea kwa nguvu kwa Senegal katika kipindi cha pili, kilichoisha kwa kiungo wa Tottenham Pape Matar Sarr kufunga bao la ushindi.

Ushindi wa Senegal dhidi ya Sudan Kusini ugenini na nyumbani dhidi ya Mauritania mwezi Oktoba utawapa tiketi ya tatu mfululizo ya Kombe la Dunia.

Nigeria matatani 
Nigeria wako hatarini kukosa Kombe la Dunia kwa mara ya pili mfululizo baada ya kutoka sare ya 1-1 ugenini dhidi ya vinara wa Kundi C Afrika Kusini mjini Bloemfontein.

Mabeki wa Super Eagles walifunga mabao yote mawili kipindi cha kwanza: nahodha William Troost-Ekong akijifunga, kisha Calvin Bassey kusawazisha kwa kichwa.

Nigeria wako nyuma ya Afrika Kusini kwa pointi sita, na matumaini yao ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 Amerika Kaskazini huenda yakategemea kumaliza nafasi ya pili na kufuzu mchujo.

Misri wasubiri kidogo 
Ushindi ungeihakikishia Misri kufuzu kutoka Kundi A, lakini walilazimishwa sare ya 0-0 na Burkina Faso walioko nafasi ya pili. Pharaohs wanahitaji pointi mbili zaidi kufanikisha kufuzu kwa mara ya nne.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending