Connect with us

News

Dkt. Nzai, awahimiza vijana kujisajili kwa mpango wa elimu kwa wote

Published

on

Kama njia mojawapo ya kuimarisha vijana wa Pwani kupitia elimu, Jumuiya ya kaunti za Pwani imeanzisha mpango wa elimu kwa wote unaotoa elimu ya juu kupitia mtandao.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya kaunti za Pwani, Dkt. Emmanuel Nzai alisema wanalenga vijana elfu tano kupitia mpango huo huku idadi lengwa ya vijana wa kaunti ya Kilifi ikiwa 700.

Dkt. Nzai alitoa wito kwa vijana kujisajili kwenye mpango huo ikizingatiwa kwamba ni vijana 25 pekee katika kaunti ya Kilifi ambao tayari wamejisajili kwenye mpango huo.

Dkt. Nzai alidokeza kwamba wanashirikiana na taasisi ya kimataifa ya Regeneysis kufanikisha mpango huo.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu kaunti ya Kilifi Felkin Kaingu alisema kupitia wafadhili mbalimbali watahakikisha kuwa vijana watakaojisajili kwenye mpango huo wanafadhiliwa kuendeleza masomo yao.

Hata hivyo vijana ambao tayari walinufaika na mpango huo walisisitiza haja ya hamasa zaidi kutolewa kwa vijana hasa wa mashinani ili wapate kujua kuhusu mpango huo wa elimu kwa wote.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending