Connect with us

News

Gachagua, amkosoa Rais Ruto kwa madai ya uongozi duni

Published

on

Viongozi wa upinzani nchini wakiongozwa na Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua waliendeleza kampeni za Wantam dhidi ya rais William Ruto wakielenga uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.

Wakazingumza wakati wa ziara yao ya kisiasa katika eneo la Pwani, Kalonzo alimkosoa rais Ruto akisema ameshindwa kuongoza taifa hali na kuendelea kuwanyanyasa vijana wa Gen Z kwa kuwateka nyara kiholela.

Kalonzo hata hivyo alidai kwamba serikali ya Kenya kwanza ina malengo fiche dhidi ya Bandari ya Mombasa, akisema kama wapinzani watahakikisha serikali ya rais Ruto ina hudumu kwa muhula moja pekee.

“Rais Ruto alishindwa kuongoza nchi na kuendelea kuwanyanyasa wakenya hasa vijana wa Gen Z kwani tumeshuhudia utekaji nyara wa kiholela na hata bandari ya Mombasa wako na malengo fiche na hiyo”, alisema Kalonzo.

Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na ambaye pia ni Kinara wa Chama cha DCP, amemkosoa rais Ruto na Katibu wa Muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli kwa kuwahadawa wakenya na kusambaratisha uchumi wa nchi pamoja na kufuja fedha za hazina ya NSSF huku Atwoli akilinyamazia suala hilo.

“Pesa ya NSSF imechukuliwa na Rais Ruto na kuendelea kujenga barabara na Bomas hiyo ni kinyume na sheria na hatutakubali na yule kiongozi wa kutetea wafanyikazi Atwoli amenyamaza ama wamekula hiyo pesa pamoja”, alisema Gachagua.

Upinzani waendeleza kampeni za Wantam

Hata hivyo viongozi walioandamana na Kalonzo katika ziara hiyo ya kisiasa eneo la Pwani wakiongozwa na Mgombea wa kiti cha ubunge wa eneo bunge la Magarini Furaha Chengo Ngumbao, walisema serikali imesheheni wizi wa mashamba ya wakaazi wa Pwani na kudia kwamba mamlaka yote yako nchini ya wananchi.

Wengine walioandamana na Kalonzo ni pamoja na Naibu Kinara wa DCP Cleophas Malala, Mbunge wa Wundanyi Danson Mwashako, Seneta wa Kisii Richard Onyonka miongoni mwa viongozi wengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending